Naibu Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Mwamini Malemi (kulia) akizungumza na uongozi na watendaji wa Wilaya ya Kibondo mkoani Kigoma alipofanya ziara wilayani humo kwa ajili ya kukagua Kambi ya Nduta wilayani humo pamoja na Kambi za Mtendeli na Karago wilayani Kakonko ambazo zipo katika maandalizi ya kuwapokea wakimbizi wa Burundi wanaohifadhiwa kwa muda katika Kambi ya Nyarugusu mkaoni humo. Katikati ni Mkuu wa Wilaya ya Kibondo, Ruth Msafiri.
Watoto wa Wakimbizi kutoka Burundi wakiwa katika Kambi ya Wakimbizi ya Nduta ambapo wanahifadhiwa.
Baadhi
ya mahema yanayojengwa katika Kambi ya Wakimbizi ya Nduta wilayani Kibondo
mkoani Kigoma ambayo yatatumika kuwahifadhi wakimbizi kutoka Burundi
wanaoendelea kuwahamishiwa kambini hapo kutoka Kambi ya Nyarugusu ambapo
walikuwa wamehifadhiwa kwa muda.
Picha zote na Wizara ya Mambo ya
Ndani ya Nchi.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...