Siku moja baada ya kunaswa mashine zilizosadikiwa kuwa ni za uandikishaji wapiga kura kwa njia ya kielektroniki (BVR), zilizokuwa zikiandikisha wafanyakazi wa Kiwanda cha MM Steel jijini Dar es Salaam, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imeibuka na kueleza kuwa mashine hizo ni 'feki' na wala hazihusiani kwa namna yoyote na vifaa vyao.
Jaji mstaafu Damian Lubuva akizungumza na viongozi wa Chadema. Kutoka kulia ni Wakili wa chama hicho, John Malya na Reginald Munisi.
Mkurugenzi wa NEC, Ramadhani Kailima, ndiye aliyetoa ufafanuzi huo wakati akizungumza na Nipashe jana kuhusiana na mashine hizo ambazo zilikamatwa juzi wakati zikiendelea kutumiwa kwa shughuli ya uandikishaji wa wafanyakazi wa kiwanda hicho kilichopo katika eneo la Mikocheni.
Wakati Polisi wakizikamata jana kwa ushirikiano na maofisa kadhaa wa NEC, tayari mashine hizo zinavyofanana na BVR zilishaandikisha wafanyakazi zaidi ya 100 wa Kiwanda cha MM Steel.
Akielezea zaidi kuhusiana na tukio hilo, Kailima alisema kuwa, mara baada ya kupata taarifa za kuwapo kwa mashine hizo, walienda kuzikagua na kubaini kuwa hazina uhusiano na zile za Biometric Voter Registation (BVR), zilizotumiwa na wao (NEC) kuandikisha wapiga kura kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 25.
“Hakuna ukweli wowote kuwa zile ni mashine za BVR na tumebaini ni feki, tena ni sawa na zile zinazotumika kwenye ofisi mbalimbali kuandikisha wafanyakazi wake... hawa waliosema ni mashine za kuandikishia wapiga kura hawako sahihi... si kweli,” alisema Kailima.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...