Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Kike Duniani Mkurugenzi wa watoto kutoka Wizara ya Jamii, Jinsia na Watoto Bi. Margaret Sawe Mussai akiwaasa watoto wa kike kuzingatia elimu kwani ndio nguzo ya msingi katika maisha yao wakati w siku ya Mtoto wa Kike Duniani iliyofanyika katika viwanja vya shule ya Tandale jijini Dar. (Picha na Geofrey Adroph wa Pamoja Blog).
Na Mwandishi wetu
WAKATI serikali imekiri kwamba pamoja na kuwa na sheria kali za kuzuia ukatili kwa watoto bado kuna matukio mengi yanayowanyima watoto uhuru na haki zao msingi,wadau mbalimbali walioshiriki tamasha la mtoto msichana wamewataka wasichana kutimiza ndoto zao.
Katika tamasha hilo lililofanyika katika shule ya msingi Tandale, wilaya ya Kinondoni mkoani Dar es salaam kuanzia saa tatu asubuhi hadi saa nane vipaji mbalimbali vya watoto vilioneshwa na watoto nao kutoa kauli zao za kutaka haki na ustawi wao kwani wao ni taifa la sasa.
Pamoja na watoto hao kutoa ushuhuda na kuonesha njia ya kusaidiwa, Mkurugenzi wa watoto kutoka wizara ya maendeleo ya jamii , jinsia na watoto Margaret Sawe Mussai pamoja na kuwaambia watoto na jamii kutumia simu 119 kuelezea ukatili, ametaka madawati yaliyopo Polisi kutumika vilivyo kukabiliana na vitendo hivyo.
Alisema lazima wazazi na walezi wawajibike katika kulinda watoto kwani taarifa zilizopo sasa haziridhishi hata kidogo.
Alisema taarifa zilizopo watoto wa kike asilimia 29 na wavulana asilimia 13 wamenyanyaswa kijinsia wakati wasichana asilimia 14 na wavulana asilimia 6 wamekabiliwa na tatizo la kujaribiwa kuvurugwa kijinsia.
Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia idadi ya watu duniani (UNFPA) Bi. Natalia Kanem akizungumza jambo kwenye siku ya Mtoto wa Kike Duniani iliyofanyika katika viwanja vya shule ya msingi Tandale jijini Dar.
Akizungumzia suala la mimba za utotoni alisema kwamba wizara imeandaa program za kukabiliana na mimba na ndoa za utotoni huku akisema kwamba sheria ya ndoa ya mwaka 1971 iko mbioni kubadilishwa ili kupandisha umri wa kuolewa kuwa miaka 18.
Aidha alisema serikali na wadau wengine wanaendesha mafunzo ya kuwatoa watoto katika mazingira hatarishi pamoja na kusaidia wazazi vijana ambao walikatisha shule kutokana na ujauzito.
Mkurugenzi huyo pamoja na kueleza changamoto za malezi na ulinzi kwa watoto amesema sera zilizopo zinaendelea kuboreshwa ili kutoa ulinzi zaidi katika kuhakikisha taifa linakua na watoto wenye uhakika wa usalama.
Naye Mwakilishi Mkazi wa Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia Idadi ya watu UNFPA Dk. Natalia Kanem alisema mtoto msichana anahitaji kushikilia ndoto yake pamoja na changamoto zinazojitokeza.
Alisema pamoja na kuwepo kwa vikwazo vya mawasiliano , mtoto wa kike anastahili kupewa taarifa mbalimbali zinazomweka huru katika mambo ambayo yanamhusu yeye na jamii yake.
Alisema pamoja na haja ya kuwepo kwa usawa wa kijinsia, mtoto wa kike ni lazima apate haki yake ya kusoma,kutodhuriwa na utamaduni uliopitwa na wakati ambao ni kandamizi kama kukeketwa na ndoa za utotoni na kutobaguliwa.
Watoto wa kike wakionesha vipaji katika mpira wa miguu wakati wa siku ya mtoto wa kike Duniani.
KWA PICHA ZAIDI BOFYA HAPA.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...