Na Beatrice Lyimo-Maelezo
SERIKALI imesema itaendeleza uhusiano na ushirikiano wake na Jamhuri ya Watu wa China kwa kuimarisha  fursa mbalimbali za kijamii ikiwemo nyanja ya  kiutamaduni. 

Hayo yamesemwa leo Jumatatu (Oktoba 12, 2015)Jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi wa Idara ya Habari Bw. Assah Mwambene wakati wa halfa ya uzinduzi wa chaneli mpya ya filamu ya China –Africa Movies itakayoonyeshwa kupitia kituo cha televisheni cha Easy Television kilichopo nchini.

Bw. Mwambene amesema kuwa uwepo wa chaneli hiyo utasaidia wazalishaji wa Tanzania kuonekana na kujulikana kimataifa na kuweza kujiongezea kipato na fursa kwa waandaaji hao.

“Chaneli hii itawapa fursa kwa pande zote mbili kwani filamu ya Tanzania itaonyeshwa china na kutafsiriwa kwa lugha yao na kwa upande wa Tanzania filamu za china zitaonyeshwa hapa Tanzania na kutafsiriwa kwa lugha ya Kiswahili”

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...