Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akisalimiana na Viongozi mbali mbali wa Serikali wakati alipowasili katika uwekaji wa jiwe la Msingi ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo,ujenzi wa jengo hilo unajengwa na Kampuni kutoka China
Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohamed Shein akifungua pazia kama ishara ya uwekaji wa Jiwe la msingi ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II linalojengwa na kampuni kutoka China katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar leo,(katikati) Naibu waziri wa Miundombinu na Mawasiliano Issa Haji Ussi (GAVU)
Misimamizi wa Mradi kwa upande wa Serikali ya Mapinduzi Yasser De Costa katika Ujenzi wa jengo jipya la Abiria Terminal II linalojengwa na kampnuni ya Kichina katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar akitoa maelezo ya maendeleo ya ujenzi huo alipotembelea baada ya kuweka jiwe la msingi leo katika uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume Zanzibar.
[Picha na Ikulu.]
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...