Mtuhumiwa wa makosa ya mtandao anayetuhumiwa kusambaza katika mitandao taarifa za uongo zinazomhusu Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na usalama, Benedic Angelo Ngonyani (24) (wa kwanza Kulia) akiwa katika mahakama ya hakimu mkazi ya Kisutu akisubiri kusomewa mashtaka.
Wengine ni watuhumiwa wa wizi kwa kutumia mitandao ya simu (fraud and use of telecommunication network) Ally Hamze (53) raia wa Afrika Kusini(wa Pili kulia), Huang Kun Bing (26)Raia wa China (wa Tatu Kulia) Irfan Mirza Baig (46) (wa kwanza Kushoto) Hefeez Irfan (32)(wa pili kushoto) na Mirza Rizwan Baig(41) (wa tatu kushoto) wote watatu raia wa Pakistani wakiwa katika Mahakama ya hakimu mkazi Kisutu wakisubiri kusomewa mashtaka ya Uwizi kwa kutumia mitandao ya simu (fraud and use of telecommunication network).
Kesi zote zimeahirishwa hadi Oktoba 23, watuhumiwa wote wamepelekwa rumande huku uchunguzi ukiendelea.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...