Mwenyekiti  wa Kamati ya maandalizi ya tamasha la kumshukuru mungu kwa amani na utulivu wakati wa uchaguzi mkuu, Alex Msama akifafanua jambo wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, leo, kuhusu maandalizi ya tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika Desemba 25 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar na kuwahusisha waimbaji mbalimbali wa nyimbo za kiroho kutoka ndani ya nje ya nchi. Kushoto ni Mratibu wa tamasha hilo, Khamis Pembe.

 KANISA la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) mkoani Dodoma limewataka waandaaji wa Tamasha la Kushukuru, Kampuni ya Msama Promotions kuukumbuka mkoa wa Dodoma katika tamasha hilo linalotarajia kufanyika Desemba 25 katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es Salaam.

Akizungumza  mwishoni wa wiki jijini Dar, Mwenyekiti  wa Kamati ya maandalizi ya tamasha hilo,Alex Msama alisema amepokea taarifa hiyo kutoka kwa Mchungaji wa kanisa hilo mkoani Dodoma, Elia Meshack.

Msama alisema Mchungaji Meshack ameliomba tamasha hilo ili kufikisha asante yao kwa Mungu baada ya kufanikisha uchaguzi Mkuu wa Tanzania uliofanyika Oktoba 25 nchini kote.

Aidha Msama kwa kuwa waliandaa tamasha la kuombea amani uchaguzi Mkuu, hapana budi kurudisha shukrani kwa Mungu baada ya kuomba amani katika uchaguzi huo.

“Nimezungumza na Mchungaji Meshack akinieleza kwamba itakuwa vema Tamasha la Shukrani nikilifikisha mkoani Dodoma, Kamati yangu inafanya mikakati ya kuweza kufikisha asante kwa Mungu,” alisema Msama.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...