Na Bashir Yakub
Kesi/shauri  lolote  iwe  jinai  au  madai  kuishinda  kwake   mara  nyingi  hutegemea  mambo  makuu  mawili. Kwanza  mashahidi ,pili  ushahidi. Mashahidi  siku  zote  ni  watu.  Hakuna  kitu  kinaweza  kuitwa  mashahidi  halafu  kisiwe  binadamu. 
Hii ni  tofauti  na  ushahidi. Ushahidi   si  lazima  wawe  binadamu.   Vitu hasa  vizibiti(exhibit)  ndivyo  huitwa  ushahidi. Nyaraka, mali,  vifaa,  na  kila  kitu  ambacho  mtu  anaweza kukitumia  mahakamani kuthibitisha  kile  anachokisema huitwa ushahidi. 
Yumkini  yawezekana  wakati  huohuo  mmoja  ukawa  na  vyote  yaani  ushahidi  pamoja na  mashahidi  hapohapo.  Hii  hutegemea namna mtu  alivyojiandaa  katika    kuwasilisha  kesi  yake.

1.SIFA  ZA  SHAHIDI.
Si  kila  mtu  ana  sifa  za  kuwa  shahidi. Shahidi  hutakiwa  kuwa  mtu  mkweli , muaminifu  na  muadilifu.  Lakini  pia  sifa  kuu  ya  shahidi  ni  kuwa  na  akili  timamu.  Mtu  asiye  na  akili  timamu  hawezi  kuwa  shahidi. Lakini  pia  mtu  mwenye  sifa   ya  uongo  hasa  huko  nyuma  kama  aliwahi  kutoa  ushahidi  wa  uongo  mahakamani  na  ikathibitishwa  kuwa  alitoa  ushahidi  wa  uongo   basi  naye  hupoteza  sifa  ya  kuwa  shahidi.  
Pia  sifa  nyingine  kuu  ya  shahidi   ni  muhimu  awe  ni  yule  aliyeona,  kuhisi  kwa  kutumia  moja  kati  ya  viungo  vyake,   au  kusikia .  Hii  ina  maana  shahidi  hutakiwa kuwa yule  anayelijua  tukio  kwa  kulishuhudia  na  si  vinginevyo

2.  IDADI  YA  MASHAHIDI  INAYORUHUSIWA.
Hakuna  idadi  ya  mashahidi  rasmi  inayoruhusiwa  kisheria.  Idadi  yoyote  ya mashahidi  inaruhusiwa.  Suala  la  msingi  hapa  ni  kuwa  kila  shahidi  katika  mashahidi  hao  unaowaleta  awe  na  umuhimu  katika  kesi.  Usilete  watu  ambao   hawahusiki  na  kuisababishia  usumbufu  mahakama. Hii  ni  kwasababu  wingi  wa  mashahidi hauakisi  ushindi  katika  kesi. Hata  shahidi mmoja  tu  kama  ni  wa  muhimu anaweza  kukufanya  ushinde  kesi na kumshinda  mwenye  mashahidi  ishirini.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...