Na  Bashir  Yakub.

Ardhi  inaweza  kumilikiwa  na  mtu  zaidi  ya  mmoja. Inaweza  kuwa  nyumba  au  kiwanja.  Vyote  hivi  vinaweza  kumilikiwa  na  mtu  zaidi  ya  mmoja. Kumiliki ardhi  kwa  zaidi  ya  mtu  mmoja  sio  lazima  iwe  kwa  wanandoa. Inaweza  kuwa  ndugu ,  marafiki ,  kikundi  cha  watu kama  wafanyabiashara, wana  saccos, kikundi  cha  michezo  na  aina  yoyote  ya  kikundi  cha  kimaendeleo.  Umiliki  wa  ardhi  kwa  pamoja  unatofauti  na  umiliki  binafsi  yaani umiliki wa  mtu  mmoja  mmoja. Tutaona  tofauti  hizo   na  mambo  mengine  ya  msingi  kuhusu  umiliki  wa  pamoja.

1.AINA  ZA  UMILIKI  ARDHI.
Kwa  kuangalia  ardhi  katika  mrengo  wa  umiliki   tunaweza  kusema   kuwa  ardhi  humilikiwa  kwa  namna   mbili.  Kwanza  umiliki  wa  mtu  mmoja  mmoja   na  pili  umiliki  wa  pamoja.  Huu  ni  ule  niliosema  kuwa  ni  mtu  zaidi  ya  mmoja. 

Umiliki  binafsi  wa  ardhi  yaani  umiliki  wa mtu mmoja  mmoja   unatoa  haki  kwa  mmiliki  huyo   kuitumia  ardhi  bila  kuhitaji  ridhaa  ya  mtu  mwingine  yoyote. Anaweza  kuuza,  kuweka  rehani  kama  dhamana  ya  mkopo, kutoa  zawadi,  kupangisha  na  matumizi  mengine  yoyote  halali.  Atafanya  yote  haya  bila  kuhitaji ridhaa  ya  mtu  mwingine  yoyote.

Hii  ni  tofauti  na  umiliki  wa  ardhi   wa  pamoja.  Katika umiliki  wa  aina  hii   mtu  mmoja  hawezi  kuuza, kutoa  zawadi,  kuweka  rehani  kupangisha  au   kuruhusu  matumizi  ya  ardhi   kwa  namna yoyote ile  bila  ridhaa  ya  wengine.  Kama  ni  wawili  basi  ridhaa  itabidi  itokane  na  wawili  lakini  pia  kama  ni  kumi,  saba  ,  watano  au  zaidi  basi  ridhaa  yao  wote  itatakiwa  kabla  ya  kufanyika  kwa  muamala  wowote ule.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...