Kikosi cha timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ inayodhaminiwa na bia ya Kilimanjaro Premium Lager kimewasili salama nchini Algeria jana jioni majira ya saa 10, kabla ya kuanza safari ya kuelekea katika mji wa Bilda.

Msafara wa Taifa Stars unaongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji, Athumani Kambi, ambapo jumla ya watu 40 wapo katika mji wa Bilda wakiwemo wachezaji 21 wanaojiandaa kwa mchezo wa marudiano.

Mara baada ya kufika katika uwanja wa ndege Algiers, Stars ilipokelewa na watanzania na wanafunzi wanaoshi nchini Algeria, na kuongozana na timu mpaka katika mji wa Bilda ilipofikia timu.

Stars imeanza kufanya mazoezi leo saa 1 jioni katika uwanja wa Mustapha Tchaker utakaotumika kwa mchezo wa marudiano siku ya Jumanne.

Katika mchezo wa awali uliochezwa jana jioni jijini Dar es salaam, Tanzania ilitoka sare ya mabao 2 – 2 dhidi ya Algeria, hivyo kuifanya Stars kusaka ushindi katika mchezo wa marudiano ili kuweza kusonga mbele.

Kocha wa Taifa Stars, Charles Mkwasa amesema vjana wake wote wapo katik ahali, hakuna majeruhi na wapo tayari kwa ajili ya kusaka ushindi siku ya Jumanne, na kusema makosa yaliyojitokeza katika mchezo wa jana wanayafanyia kazi yasijitokeze tena katika mchezo unaofuata.

Taifa Stars imefikia katika hoteli ya Ville Des Roses imetumia takriabn muda wa saa 1 kutoka katika uwanja wa Ndege wa Algiers mpaka katika hoteli hiyo iliyopo eneo la Bilda.

Namba ya simu ya Afisa Habari wa TFF aliyeambatana na timu nchini Algeria +213 558 465069

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Usoni mbona kama wa hofu! au ni hasira za kuumiza mtu?!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...