Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania yasaini mkataba wa jumla ya Euro milioni 158.5 na Serikali ya Ujerumani wenye lengo la kusaidia Bajeti ya Serikali pamoja na msaada wa kiufundi.
Hayo yamesemwa na Katibu Mkuu Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelie aliposaini mkataba huo na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Egon Kochanke leo jijini Dar es salaam
Dkt. Likwelile alisema kuwa lengo kuu la fedha hizo zitaelekezwa katika sekta ya Afya, Mazingira, Nishati, Maji na kuimarisha Ofisi ya Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali.
Kwa upande wake Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Egon Kochanke alisema kuwa nchi yake itaendelea kushirikiana na Tanzania kwa kuwa nchi hizo zimekuwa na uhusiano mzuri wa muda mrefu ambao umekuwa na manufaa na tija kwa wananchi baina ya nchi hizo mbili.
Katibu Mkuu Wizara ya
Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile (kulia) akifurahia
jambo na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Egon Kochanke (kushoto) wakati
wa maandalizi ya kusaini mkataba utakaoipatia Tanzania jumla ya Euro milioni
158.5 kusaidia Bajeti ya Serikali pamoja na msaada wa kiufundi.
Katibu Mkuu Wizara ya
Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile (kulia) akibadilishana
mkataba na Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Egon Kochanke mara baada ya
kusainiwa leo jijini Dar es salaam.
Ujumbe ulioshuhudia
utiaji saini utakaoipatia Tanzania jumla ya Euro milioni 158.5 kusaidia Bajeti
ya Serikali pamoja na msaada wa kiufundi. Wa pili kutoka mwisho ni Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile, kulia
kwake ni Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Egon Kochanke, Mshauri wa
Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bi. Claudia Imwolde-Kraemer, Afisa
Msimamizi wa Fedha Wizara ya Fedha Bw. Abdallah Lyangu, Mchumi kutoka Ubalozi
wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Jan-Dieter Gosink na kushoto kwa Katibu Mkuu
Wizara ya Fedha ni Mchumi Wizara ya Fedha Bw. Melckzedek Mbise kwenye picha ya
pamoja mara baada ya kumalizika kwa hafla hiyo iliyofanyika Wizara ya Fedha.
Katibu Mkuu Wizara ya
Fedha na Mlipaji Mkuu wa Serikali Dkt. Servacius Likwelile (kushoto) akifafanua
jambo kwa ujumbe wa Ujerumani mara baada ya kusaini mkataba utakaoipatia
Tanzania jumla ya Euro milioni 158.5 kusaidia Bajeti ya Serikali pamoja na
msaada wa kiufundi. Kulia kwake ni Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bw. Egon
Kochanke, Mshauri wa Balozi wa Ujerumani nchini Tanzania Bi. Claudia
Imwolde-Kraemer pamoja na Mchumi ubalozi wa Ujerumani nchini Tanzania
Bw.Jan-Dieter Gosink.
Msipende mikopo na hatutaki kumtia kwenye kitanzi Rais wetu mchapa kazi sisi tunataka kuona Tanzania inayo jitegemea kutokana na mari tulizo nazo kuanzia kesho chini ya MAGUFULI Tanzania bila ya mikopo inawezekana, wabunge bila ya magari ya kifahari inawezekana, Tanzania bila ya maduka ya Madawa mitaani inawezekana tunataka Madawa yote yapatikane kwenye hospital za serikali tu, Tanzania bila ya magari ya kifahari kwenye wizara zote inawezekana na hatutaki tena au kuona Mama zetu na Madada zetu wakiteseka kwenye hospital zote ndani ya Tanzania yetu. ni mimi wenu The mdudu aka muona mbali
ReplyDeleteHizo pesa zingetumika kuwapa wanafunzi mikopo mnazani watasomaje tumechoka kusubiri wakati wengine wapo chuo tayari
ReplyDeleteHizo pesa zitumike kuwapa mikopo wanafunzi tunapata shida na wengine hatujaenda chuo mpka sasa kwasababu hatuna ada serikal itufikirie kwa kweli tunasomaje sasa asilimia kubwa ni watoto wa wakulima ina maana hatuna haki ya kusoma na kupewa mikopo?
ReplyDelete