Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo (kulia) akimsikiliza Meneja wa Kampuni ya GASCO, Mhandisi Mhandisi Kapuulya Musomba (katikati). Wa Kwanza kushoto ni Naibu Katibu Mkuu, Mhandisi Paul Masanja.
Kituo cha Kuchakata Gesi Asilia cha Madimba
Baadhi ya mitambo kwenye Kituo cha kuchakata Gesi Asilia cha Madimba.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Mhandisi Omar Chambo (kushoto) na Naibu wake, Mhandisi Paul Masanja mara baada ya kukagua Kituo cha Kuchakata Gesi asilia cha Madimba.
Wataalamu wa Kitanzania wanaofanya kazi kweye Mradi Mkubwa wa Gesi Asilia nchini wametakiwa kuhakikisha wanajifunza kwa ukamilifu shughuli zote za mradi huo kabla mkandarasi hajaondoka.
Wito huo umetolewa hivi karibuni na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati, Mhandisi Omar Chambo na Naibu wake, Mhandisi Paul Masanja walipofanya ziara kwenye mradi huo kwa lengo la kukagua maendeleo ya mradi pamoja na kuzungumza na wafanyakazi wa mradi huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...