Tarehe 11 Desemba, 2015, filamu iliyokuwa ikisubiriwa kwa hamu kubwa, “Going Bongo” itaanza kuonyeshwa katika jumba la sinema la Cinemax Century lililopo Mlimani City katika jiji la Dar-es-sallam. 
Filamu hiyo ambayo imetengenezwa Tanzania and katika jiji la Los Angeles kule Marekani inamhusu daktari wa kimarekani anayekuja kimakosa kufanya kazi Tanzania kwa muda wa mwezi mmoja. 
Filamu hii imekwishajishindia tuzo mbali mbali za kimataifa ikiwemo, filamu bora ya Afrika Mashariki (ZIFF) na filamu bora ya kimataifa (BEFFTA). 
Mwandishi/Mtayarishaji/Muigizaji wa filamu hiyo Ernest Rwandalla (Ernest Napoleon) amesema kuwa tiketi za maonyesho ya saa 12 jioni, saa 2 na saa 4 usiku za Ijumaa tarehe 11 Desemba, zimeshaanza kuuzwa pale Mlimani City. Going Bongo ni filamu inayotararijiwa kufanya vizuri katika majumba ya sinema ambayo yamekuwa yakionyesha zaidi filamu za nje.

For  more  inquiries  please  contact:

Mr. Ernest-TEL +46704070827(Whats app)
Da June-TEL 0756735461

GASTON TEL 0715241177

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...