Kaimu Mkurugenzi wa KADCO ,Bakari Murusuri |(Katikati) kushoto kwake ni mkurugenzi wa shughuli mama za kiwanja na huduma KADCO,Christopher Mukoma na kulia kwake ni Meneja usalama wa Kiwanja, Justine Kisusi walipokutana na wanahabari .
Kaimu mkurug4e3nzi wa KADCO ,Bakari Murusuri akizung4umza na wanahabari (hawako pichani ) kuhusu matukio mbalimbali yaliyojitokeza katika uwanja huo. 
Uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA)
Eneo la ndani la uwanja wa ndege wa KIA.
…………………………………………………………..


Na Dixon Busagaga wa Globu ya Jamii Kanda ya Kaskazini., 

KAMPUNI ya maendeleo ya viwanja vya ndege (KADCO) inayosimamia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) imekoa zaidi ya kiasi cha sh Bil 2 katika kipindi cha wiki moja ikiwa ni thamani ya nyara za serikali na vito vya thamani vilivyokuwa vitoroshwe kupitia uwanja huo. 

Menejimenti ya uwanja huo kupitia kitengo cha usalama kiwanjani hapo ilifanikiwa kukamata kunasa vipande 264 vya madini ya Tanzanite vikiwa na uzito wa kilograamu 2.04 ambavyo thamani yake inakadiriwa kufikia Bilioni 2.5. 

Vingine vilivyokamatwa uwanjani hapo vikiwa njiani kusafirishwa kuelekeaa nchini Vietnam ni pamoja na kucha 261 ,meno 60 ya Simba ambayo yanadaiwa kutokana na kuuawa kwa Simba 13 . 
Kaimu mkurugenzi wa KADCO,Bakari Murusuri aliiambia Globu ya jamii kuwa Desemba 18 ,maofisa usalama uwanjani hapo walimkamata abiria mwenye asili ya Uarabuni akiwa na pembe mbili za Twiga. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...