Mahafali ya tisa ya Taasisi ya Teknolojia Dar es Salaam (DIT), yanatarajiwa kufanyika Jumamosi 30 Januari mwaka 2016 na yatatanguliwa na utoaji tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri katika mwaka wa masomo 2014/2015.
Sherehe hizo za utoaji wa tuzo kwa wahitimu waliofanya vizuri, zitafanyika mapema 22 Januari mwaka 2016 katka viwanja vya chuo hicho kikongwe cha masuala ya teknolojia nchini.
Taarifa kwa vyombo vya habari iliyotolewa na taasisi hiyo, inawafahamisha wahitimu wote wa mwaka wa masomo 2014/2015, kusoma utaratibu wa kuthibitisha kushiriki mahafali hayo katika tovuti ya Taasisi www.dit.ac.tz.
Wahitimu hao ni wale wa Shahada ya Uzamili (M.Eng), Shahada ya  kwanza ya Uhandisi (B.Eng.) na  wahitimu wa Stashahada ya Uhandisi (OD) na “Rehearsal” kabla ya mahafali itafanyika Ijumaa tarehe 29/01/2016.
Taarifa hiyo imewataka wahitimu watakaoshiriki kulipia joho la mahafali Tshs 50,000/= (kwa wahitimu wa Shahada ya Uzamili - M.Eng) na  Tshs 30,000/= (kwa wahitimu wa Shahada ya kwanza (B.Eng) na Stashahada (OD).
Wahitimu wametakiwa kulipa fedha hizo  katika tawi lolote la NBC  kwenye akaunti namba 018101003145 na kujisajili kupitia tovuti ya Taasisi www.ac.dit.tz
Taarifa hiyo imebainisha kuwa wahitimu wanatakiwa kuwa makini na kuhakikisha malipo yamefanyika kwa kutumia jina kamili kama linavyoonekana kwenye orodha ya wahitimu wa mwaka 2014/15 iliyopo kwenye tovuti ya Taasisi.

Pia yaonyesha namba ya usajili na madhumuni ya malipo (yaani mahafali) na mwisho wa kujisajili ni 31 Desemba, 2015 na wahitimu wanahimizwa kupeana taarifa kuhusiana na mahafai hayo ya tisa ambayo mgeni rasmi atatangazwa baadae.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...