Makamu Mkuu wa Chuo Kikuu cha Ardhi Prof. Idrisa Mshoro akimkabidhi cheti mmoja wa wanafunzi wa mwaka wa nne aliyefanya vizuri katika masomo yake kwa mwaka 2014/2015  wakati wa leo jijini Dar es salaam.
 Naibu Makamu Mkuu wa Chuo anayeshughulikia masuala ya Taaluma wa Chuo Kikuu cha Ardhi Prof. Gabriel Kassenga akizungumza na wanafunzi na wageni mbalimbali waliohudhuria hafla ya utoaji wa Tuzo kwa wahitimu wa chuo hicho waliofanya vizuri leo jijini Dar es salaam.
  Baadhi ya Wahadhiri wa Chuo Kikuu cha Ardhi, wawakilishi wa Makampuni na Taasisi mbalimbali waliochangia tuzo mbalimbali na Wahitimu wa miaka ya nyuma wa Chuo hicho wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa hafla fupi ya utoaji wa Tuzo kwa wanafunzi waliofanya vizuri leo jijini Dar es salaam.
  Wahitimu wa Chuo Kikuu cha Ardhi waliofanya Vizuri waendelea kupokea tuzo zao. Takribani wanafunzi 126 wamepata Tuzo na zawadi mbalimbali wakiwemo wanafunzi kike 61 waliofanya vizuri katika masomo ya Sayansi.
 Wanafunzi na Wageni mbalimbali waliohudhuria hafla hiyo
 Mwanafunzi Bora wa Kike wa Chuo Kikuu cha Ardhi katika fani ya Upimaji wa Ardhi ( Geomatics) Bi. Lilian Kato akipokea zawadi yake ya mashine ya kupimia Ardhi (Total Station) yenye thamani ya shilingi milioni 15 aliyozawadiwa na Kampuni ya High Tech Systems kwa kuwa mwanafunzi bora wa kike wa mwaka wa nne kwa mwaka 2014/2015
Kwa picha zaidi BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...