Baada ya kufanikisha kwa Tamasha la siku ya Kandanda hapo Oktoba 17 mwaka jana, Tamasha lililobeba Ujumbe wa "#OneBallOnTxt Book" ikiwa ni Dhima kamili ya kunyanyua Mchezo wa mpira wa miguu kuanzia ngazi ya shule ya msingi na kuwasisitizia watoto wetu umuhimu wa kusoma pia, Timu nzima ya Wanakandanda imeonelea Kuufungua Mwaka 2016 kwa kwenda kutembelea Kituo cha kulelea watoto wanaoishi kwenye mazingira magumu na kukabidhi Mchango wao ambao ulitokana na mauzo ya fulana za Tamasha la Siku ya Kandanda mwaka jana.
Ikumbukwe tulieleza kwamba kwa kila Fulana moja itakayonunuliwa, asilimia kumi itaenda katika kampeni ya #MpiraMmojaKitabuKimoja (#OneBallOneTxtBook). Kamati ilifanikiwa kuuza Fulana 100 ambazo tumefanikiwa kutumia asilimia iliyotakiwa katika kununulia vifaa ambavyo tunakabidhi  katika kituo cha House of Blue Hope Leo hii.
Vitabu vilivyonunuliwa ni vya Hisabati, Kiingereza, Kiswahili, Sayansi, Jiografia na Teknohama. Mipira imekabidhiwa miwili, ambayo tulipewa na mdhamini, hivyo pesa iliyotakiwa kununulia mipira tuliongezea katika vitabu.
“Tunashukuru Kandanda Day kwa mchango huu katika kituo chetu, utasaidia kuwajenga watoto kimasomo na kimichezo” Amesema Msimamizi wa kituo hicho, Daudi Mboma.
Pia Tunachukua nafasi hii kutoa shukrani zetu za dhati kwa wadhamini wetu wote( BinSlum , BayPort TZ, SDS, Michuzi Media Group, MacAuto Accessories, SalehJembe Blog, Pepsi, GALACHA na Kandanda.co.tz) tuliokuwa nao toka Tunaanza Tamasha hili la Siku ya Kandanda kwa Mwaka wa Tatu mfululizo kwa kujitolea kwao kwetu katika kufanikisha Siku yetu pia kuwapa Mrejesho wa kile ambacho tumekifikia kwa Mwaka wa Tatu!. Pia bila kuwasahau Chama cha Madaktari, TASMA, kwa kushiriki nasi katika Tamasha la mwaka jana.
Hakika mafanikio ni mengi sana si rahisi ya kuyaorodhesha yote lakini kwa Uchache ni kukua kwa Muamko kwa Familia ya watu wa Kandanda katika ushiriki wa Siku hii, pia Kujua umuhimu wa kushiriki katika michezo kwa Jamii katika kudumisha Afya za miili yetu pamoja na kushiriki katika upimaji wa Afya zetu siku ya Tamasha.
Malengo ya Siku hii ya Kandanda ni kuinua Ari na Muamko kwa wananchi wote katika kushiriki katika matamasha na kurudisha kile ambacho jamii ya wasionacho wangekihitaji kukipata kupitia matamasha haya.
Kama Taifa mchezo upendwao zaidi ni Kandanda lakini bila Maarifa na Vifaa hatuwezi kuja kuwa na Kina Mbwana Samatta ama Thomas Ulimwengu wengi zaidi hivyo basi tunapenda tutoe Rai kwa Watanzania wote waliopo ndani na nje ya Nchi kushirikiana nasi katika kufikia malengo yetu makuu ya kupeleka Kitabu Kimoja na Mpira Mmoja katika kila Kaya ya Mtanzania mmoja ili kuinua Elimu, Michezo pamoja na kujenga  Afya ya miili yetu.
Tungependa watu wengi zaidi, kutoka katika jamii tofauti, mashirika tofauti na hata makampuni tofauti tukaungana kwa pamoja Mwaka huu 2016 na kuifanya siku hii iwe kubwa zaidi na Tupeleke na kuwafikia watoto wengi Zaidi. Tunatarajia kuwa na siku ya kandanda mwaka huu Katika siku ya Jumamosi ya Tatu ya Oktoba (#Oktoba15), ikitanguliwa na matamasha madogo madogo ambayo tutatoa utaratibu hapo baadae ili kuwapa wadau wa kandanda kote kushiriki. Lengo letu ni kuhusisha Tamasha hili kufanyika siku moja katika sehemu mbalimbali Tanzania, tukiwa na lengo moja.
Kwa kuwapelekea Kitabu Kimoja na Mpira Mmoja
Pamoja Tutaweza

Kamati ya Maandalizi Kandanda Day 2015
Mwenyekiti wa Kamati, Patrick 'Patoo' Dumulinyi, akimkabidhi vitabu na mpira Mlezi wa kituo cha House of Blue Hope, Daudi Mboma. Kulia kwa Patoo ni Bi Fatma Hassan mwakilishi wa TeamDizoMoja na Kushoto kwa Mboma ni Meneja wa TeamIsmail (Mabingwa 2015/16), Ismail Mohammed.
 Picha ya Pamoja na baadhi ya watoto wa Kituo cha House of Blue Hope wakiwa na vitabu na mpira.

 Bi Fatma (Team DizoMoja) akiwa na Msimamizi wa Kituo, Daudi Mbnoma.
 Mwenyekiti wa Kamati, Patrick 'Patoo' Dumulinyi, akimkabidhi vitabu na mpira Mlezi wa kituo cha House of Blue Hope, Daudi Mboma. Kulia kwa Patoo ni Bi Fatma Hassan mwakilishi wa TeamDizoMoja na Kushoto kwa Mboma ni Meneja wa TeamIsmail (Mabingwa 2015/16), Ismail Mohammed.
  Watoto wa kituo cha House of Blue Hope wakifurahia mpira

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...