Zaidi ya wanafunzi 5,100 wa shule za msingi Wilayani Mufindi Mkoani Iringa, wanatarajiwa kujiunga na kidato cha kwanza baada ya kufaulu mtihani wa darasa la 07 ulifanyika mapema mwaka jana, huku ufaulu huo ukipanda na kufikia asilimia 80.39 ukilinganisha na asilimia 68.21 ya mwaka 2014.
 Taarifa ya kitengo cha habari na mawasiliano cha halmashauri ya wilaya ya mufindi kwa nyombo vya habari, imetanabaisha kuwa, wanafunzi waliokuwa wamesajiliwa   kufanya mtihani walikuwa 7,220 na miongoni mwao waliofaulu na kuchaguliwa kuendelea na masomo ya sekondari ni 5,198.
Taarifa hiyo imeainisha mgawavyo wa wanafunzi hao kwa kuzingatia jinsi, ambapo kati ya waliofaulu, wasichana wameongoza kwa takwimu za ufaulu huo wakiwa elfu 2,831 wakifuatiwa na wavulana 2,367. Aidha, wanafunzi wote waliofaulu wamepangiwa shule ili kuendelea na elimu ya sekondari itakayokuwa ikitolewa bure hapa nchini.
Wilaya ya Mufindi yenye jumla ya shule za msingi 178 imeshika nafasi ya pili Mkoani Iringa kwa kufaulisha wanafunzi wengi kwaasilimia 80.39 ikitanguliwa na Manispaa ya Iringa iliyofaulisha kwaasilimia 80.55 ikiwa na jumla ya shule za msingi 50.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Siku hizi darasa la saba wadogo wadogooo. Zamani tulikuwa na wenye ndevu na ma-repeater. Mtu anarudia darasa la saba zaidi ya mara nne kwa majina tofauti!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...