Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (katikati) akiwa katika kikao na watendaji wa Wizara ya Nishati na Madini, Ofisi ya Mkuu wa wilaya Tarime na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (wa pili kushoto) kilicholenga kutatua kero wanazokumbana nazo wananchi wanaozunguka mgodi wa dhahabu wa Acacia NorthMara pamoja na Mgodi husika. Kushoto kwa Waziri ni Mkuu wa wilaya ya Tarime, Glorious Luoga. Wa kwanza kulia Kamishna Msaidizi wa Madini, Kanda ya Ziwa Victoria Magharibi, Mhandisi Juma Sementa, Wa pili kulia ni Kaimu Kamishna wa Madini, Mhandisi Ally Samaje na Wa kwanza kushoto ni Kamishna Msaidizi wa Madini, Leseni,John Nayopa.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) na Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche (kushoto) wakijadiliana jambo mara baada ya kumaliza kikao kilicholenga kutatua kero za wananchi wanaozunguka mgodi wa dhahabu wa Acacia NorthMara pamoja na Mgodi husika.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (wa pili kulia) akitembelea maeneo yanayolalamikiwa na wananchi wanaozunguka mgodi wa dhahabu wa Acacia NorthMara wakati alipofanya ziara ya kikazi wilayani Tarime. Kulia kwa Waziri ni Mbunge wa Tarime Vijijini, John Heche, na kulia kwa Mbunge ni Mkuu wa wilaya ya Tarime, Glorious Luoga.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo (kulia) akimsikiliza mmoja wa wananchi wa Kijiji cha Nyakungulu wilayani Tarime ambaye alikuwa akiwasilisha kero za wananchi wanaozunguka mgodi wa dhahabu wa Acacia North Mara wakati Profesa Muhongo alipofanya ziara ya kikazi wilayani Tarime.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...