SIMU.tv: Jeshi la polisi mkoani Arusha kwa kushirikiana na raia wema limefanikisha kuua watu wawili kati ya 4 wanaosadikiwa kuwa ni majambazi wakati wakitaka kuvamia kituo cha utafiti wa kilimo. https://youtu.be/kLBUrUL9Cu4
SIMU.tv: Hospitali ya Butiama iliyoko mkoani Mara yaelezwa kukabiliwa na hali mbaya ya utoaji huduma za afya kufuatia uchakavu wa miundombinu pamoja na ukosefu wa vifaa tiba. https://youtu.be/w061iu0qI-4
SIMU.tv: Jumla ya watoto 30 wenye matatizo ya vicha vikubwa venye kujaa maji pamoja na migongo wazi wanatarajiwa kufanyiwa upasuaji mwishoni mwa wiki hii jijini Dar es salaam. https://youtu.be/CZz3UPkesOA
SIMU.tv: Rais Magufuli atoa siku 15 kwa mawaziri na wakuu wa mikoa kuhakikisha majina yote ya watumishi hewa yanaondolewa katika malipo.https://youtu.be/XoPeFVIa99Y
SIMU.tv: Jeshi la polisi visiwani Zanzibar lathibitisha kutokea kwa mlipuko wa bomu katika nyumba ya kamishina wa polisi Zanzibar na kusababisha athari kubwa.https://youtu.be/T08XsrYLe8o
SIMU.tv: Kurugenzi ya mawasiliano ya Rais Ikulu yakanusha taarifa zilizochapishwa na gazeti la Jamb leo kwamba serikali ya awamu ya 5 imewapunguzia Maraisi wastaafu ulinzi na kulitaka gazeti hilo kuomba radhi. https://youtu.be/xmT3EI-zJs0
SIMU.tv: Waziri wa Nishati na Madini Prof. Muhongo abainisha Tanzania kugundua rasilimali nyingine ya gesi asilia katika bonde la mto Ruvu mkoani Pwani.https://youtu.be/l_R8oTcKQlw
SIMU.tv: Waziri mkuu Kassim Majaliwa atoa siku 5 kwa uongozi wa mkoa wa Kagera kutoa maelezo kuhusiana na matumizi ya fedha za mradi wa ukimwi pamoja utekelezaji wa ripoti ya mkaguzi mkuu wa serikali CAG.https://youtu.be/MaBAtXUqMe8
SIMU.tv: Waziri wa ujenzi Prof. Mkame Mbarawa afanya ziara katika daraja la Kigamboni jijini Dar es salaam kujiridhisha kuwa liko katika hatua za mwisho kwa kubainisha kuwa litazinduliwa mwezi wa 4 mwaka huu.https://youtu.be/JQFqEpCGTXU
SIMU.tv: Kamati ya kudumu ya bunge ya huduma na maendeleo ya jamii imekutana na kujadili majukumu na utekelezaji wa taasisi ambazo ziko chini ya wizara ya habari, utamaduni, sanaa na michezo. https://youtu.be/c-Bv2BF5KeM
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...