Kampuni ya Dhahabu ya Geita(GGM) imeshiriki maonyesho ya  usalama na afya mahala pa kazi kwenye viwanja vya Jamhuri  mjini Dodoma.Maonyesho hayo yameratibiwa na wakala wa usalama na Afya mahala pa kazi(OSHA) kuelekea maadhimisho ya siku ya usalama na afya mahala pa kazi Duniani.
Akizungumza kuhusu ushiriki wa Geita Gold Mine(GGM) kwenye maonyesho hayo,Ofisa mawasiliano mwandamizi wa Geita Gold Mine(GGM)  Bw Theophil Pima amesema kuwa kampuni ya GGM ni mdau wa usalama na afya mahala pa kazi na ndiyo sababu ya  kushiriki maonesho hayo.
“GGM inatambua usalama ni kitu muhimu kuliko hata uzalishaji na ndiyo maana imeshaweka tamko kabisa kuwa Usalama ndicho kipaumbele chake kikubwa kuliko vyote katika shughuli zake.Tumekuwa tukishirikiana kwa ukaribu na wakala wa usalama na afya mahala pa kazi na kupatiwa vyeti mbalimbali”alisema Bw Theophil Pima na kuongeza kuwa wafanyakazi wote wa GGM  kabla ya kuanza kazi hupatiwa mafunzo maalumu ya usalama mahala pa kazi ili kuepusha ajali ambazo ni changamoto kubwa kwa migodi mingi Duniani.
Akizungumzia kauli mbiu ya maonesho hayo kuwa "Msongo wa mawazo mahala pa kazi ni changamoto yetu sote", Bw Theophil Pima amesema kuwa Kampuni ya GGM kama zilivyo kampuni zingine inayo changamoto ya baadhi ya wafanyakazi wake kuwa na tatizo la msongo wa mawazo na ndiyo maana wanayo program maalumu ya kuleta madaktari bingwa kutoa ushauri na utaalamu wa kisaikolojia kwenye hospitali yao hapo mgodini.
“Msongo wa mawazo ni changamoto kubwa kwa sababu husababisha mfanyakazi awe na mawazo na kushindwa kufanya kazi kwa ufanisi.Wakati mwingine msongo wa mawazo hasa kwa wataalamu wanaoendesha mashine migodini unaweza kusababisha ajali”alisema Bw Theophil Pima na kuwaomba watanzania mkoani Dodoma wajitokeze kwa wingi kwenye banda lao ili kuona vifaa vya kisasa vinavyotumika kwenye masuala ya afya na usalama kwenye kampuni yao.
Akizungumzia maonyesho hayo Mkurugenzi wa usalama na afya kutoka wakala wa usalama na Afya mahala pa kazi(OSHA) Mhandisi Alex Ngata amesema maonyesho kama hayo ni fursa ya kutoa mafunzo  kwa waajiri na wafanya kazi ili watambue nafasi ya afya na usalama mahala pa kazi na namna ya kukabiliana na chngamoto mbalimbali ukiwemo msongo wa mawazo.

 Afisa mawasiliano mwandamizi wa Kampuni ya Geita Gold Mine(GGM) Bw Theophil Pima akizungumza na vyombo vya habari kwenye maonesho ya usalama na afya mahala pa kazi.Pembeni yake ni Afisa Utumishi wa GGM Bw Joseph Mgire(wa kwanza kushoto) na Bw Chacha Magige ambaye ni mratibu wa masuala ya usalama mahala pa kazi GMM.Wengine ni wataalamu kutoka GGM.
 Wakazi wa Dodoma wakitembelea banda la maonyesho la Geita Gold Mine
 Bw Mohamed Mwaimu(katikati)kutoka kitengo cha dharura na uokoaji cha GGM akiwaonyesha wanafunzi wa shule ya msingi waliotembelea banda la Geita Gold Mine jinsi ya kumuokoa mtu aliyepata ajali ya kumwagikiwa kemikali mgodini.
 Mtaalamu wa afya mahala pa kazi Bw Shija Ayoub akionyesha upimaji wa kelele na vumbi kazini


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...