Kufuatia wadau wengi kuhitaji kujua hatua zitakazochukuliwa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) dhidi ya hukumu ya kesi ya rushwa Na. 75/2014 iliyokuwa ikimkabili Bw. William Mhando aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na wenzake watano.

TAKUKURU inapenda kuufahamisha umma kwamba inafanya taratibu za kukata rufaa dhidi ya hukumu hiyo iliyosomwa tarehe 14/4/2016 na Mhe. Hakimu Mkazi Hellen katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kwaniaba ya Hakimu Mkazi Mkuu Mhe. Kyey Rusema. Katika hukumu hiyo washtakiwa wote sita (6) waliachiwa huru.

Aidha, TAKUKURU inawataka wadau na wananchi kwa ujumla kutambua kwamba ni utaratibu wa kisheria kwamba upande usioridhika na hukumu iliyotolewa kukata rufaa katika Mahakama ya juu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Baadhi ya mahakimu hawajaisoma namba bado. Kesi ya wizi wa wazi wazi wa taasisi ya umma na matumizi mabaya ya madaraka ameachiwa kabisaa? Kweli Magufuli anakazi na tumwombee. Alex bura dar.

    ReplyDelete
  2. Jaji mkuu wa Tanzania tunaomba uwaangalie kwa jicho la 3 baazi ya mahakimu coz baazi ya maamuzi ya mahakimu tuna mashaka nayo coz haiingii AKILINI serikali ina pambana kuitokomeza rushwa lakini upande wa mahakama zetu bado kama hawajui nini madhara ya RUSHWA na tujiulize why serikali inakua I nashindwa kesi zikifika mahakamani? hapo pana jambo si bule

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...