Na MatukiodaimaBlog
WAZIRI wa maji na umwagiliaji mhadisi Geryson Lwenge amewaondoa hofu wananchi wa mji wa Ilula wilaya ya Kilolo mkoani Iringa kuhusu ahadi ya Rais Dr John Magufuli ya kumaliza kero ya maji katika mji huo wa Ilula kuwa itaanza kutekelezwa mwaka huu.
Alisema kuwa serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dr Magufuli ni serikali ya ukweli na uwazi na ni serikali ya hapa kazi Tu hivyo kila ilichoahidi kukifanya itafanya kwa wakati na kuwataka wananchi kuendelea kujenga imani zaidi.
Waziri mhandisi Lwenge aliyasema hayo jana katika Mgahawa wa Bunge mjini Dodoma , wakati akizungumza katika kikao chake na mbunge wa jimbo la Kilolo Venance Mwamoto na mbunge wa viti maalum mkoa wa Iringa Ritta Kabati na wawakilishi 11 wa wananchi wa mji wa Ilula waliofika bungeni mjini Dodoma kufuatilia ahadi ya maji iliyotolewa na Rais Dr Magufuli wakati wa kampeni kwa wananchi wa mji wa Ilula .
Mwamoto akishiriki na wananchi wa mji wa Ilula kukinga maji ambayo hutoka kwa mgao.
Kijana wa Ilula akichambua nyanya. Kusoma zaidi bofya HAPA. |
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...