Manufaa yanayotokana na hifadhi za taifa na vivutio vya utalii hayatoshi tu kutumika kama nyenzo ya kupunguza vitendo vya ujangili na uvamizi katika maeneo yaliyotengwa na serikali ikiwa hakutakuwa na ushirikishwaji wa kutosha na wa moja kwa moja kwa wananchi wanaoishi maeneo yanayozunguka rasilimali hizo.

Pamoja na mchango mkubwa wa utalii katika uchumi taifa na kuwepo kwa manufaa kwa vijiji vinavyozunguka hifadhi za taifa na vitutio vingine vya utalii, jamii bado imeshindwa kuzitambua faida hizo ili kushiriki kikamilifu katika kupambana na ujangili na uvamizi holela wa maeneo hayo.

Je, jitihada zinazofanywa na serikali na wadau kutoa elimu kwa jamii na kuibua fursa muhimu katika sekta hii zinatosha?

Ili kujibu swali hilo Jukwaa linalohusu masuala ya Usimamizi Shirikishi wa jamii wa maliasili mnamo Mei 26, 2016 limewakutanisha wadau wa mazingira, maliasili na utalii kujadili mambo muhimu yanayoweza kuchangia katika kufungua milango ya fursa katika sekta ya wanayamapori.
Mratibu wa Jumuiko la Maliasi Tanzania (TNRM), Faustine Ninga akifafanua jambo wakati wa Jukwaa la Masuala ya Usimamizi Shirikishi wa Jamii wa Maliasili lililofanyika Mei 26, 2016 jijini Dar es Salaam.
Demetrius Kweka kutoka Engility, (wasimamizi na waendeshaji wa mradi wa PROTECT), akizungumzia hatua mbalimbali za utekelezaji wa mradi huo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...