Ikiwa Jumamosi hii ya Juni 25, ni ya mwisho wa mwezi wafanyakazi wa hospitali ya Taifa ya Muhimbili watekeleza agizo la Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt, John Pombe Magufuli kwa kufanya usafi katika sehemu mbalimbali za hospitali ya Muhimbili jijini Dar es Salaam leo.
Baadhi ya wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wakifanya usafi LEO ikiwa ni kutekeleza agizo la rais la kufanya usafi kila mwishoni mwa mwezi.
Kutoka kulia Chindemba Lingwana, Patrick Rogath ambaye ni Mkuu Idara ya Idara ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano kwenye hospitali hiyo, Christian Mtei na Fred Felix wakifanya usafi katika jengo la utawala LEO.
Picha na John Stephen, Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH).
Jamani usafi hadi tuambiwe? Kuwepo na watu ambao ndio kazi yao kusafisha sehemu kama muhimbili na majengo mengine ya binafsi na serikali.
ReplyDelete