Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
WATANZANIA wametakiwa kuonyesha ushirikiano kwa kuchukia vitendo wanavyofanyiwa wapelestina katika nchi yao.

Hayo ameyasema leo, Shekhe Mkuu wa Shia, Ahmed Jalala wakati akizungumza na waandishi wa habari juu matembezi ya amani yatakayofanyika mwisho wa mwezi wa Ramadhan kwa ajili ya kuomba amani kwa nchi ya Palestina.

Jalala amesema kuwa nchi ya palestina haikaliki na kufanya kuongoza kuwa idadi kubwa ya wajane na yatima kutokana na mauaji yanayofanywa dhidi yao.

Amesema kuwa vyombo vya kimataifa havijaweka nia dhabiti juu ya kufanya nchi hiyo kuwa na amani kwani vitu vinavyofanya vimeanza muda mrefu lakini hakuna matokeo.

Kiongozi huyo amesema kuwa Palestina kukiwa na amani hata ugaidi unaweza kuondoka kwani tatizo la nchi hiyo ni kubwa kuliko la ugaidi unaosemwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...