Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (kushoto) akimsikiliza kwa makini Bi. Rehema Kabuye (katikati) aliyekua akilia kwa uchungu, akimsihi Waziri huyo wa Fedha na Mipango, amsaidie ili mume wake ambaye ni Nahodha wa meli ya MV Liemba pamoja na wafanyakazi wengine wa Mamlaka ya Huduma za meli mkoani Kigoma, walipwe mishahara yao ya miezi nane ili kuwaondolea adha ya maisha inayowakabili wao na familia zao
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dokta Philip Mpango (Mb), akizungumza na wafanyabiashara wa Kigoma Mjini, kuhusu masuala mbalimbali ikiwemo umuhimu wa kulipa kodi na matumizi ya mashine za kieletroniki pamoja na kuwasisitizia kutoa risiti kwa wateja wao. kushoto kwake ni Kamishna Msaidizi anayeshughulikia masuala ya kodi, Wizara ya Fedha na Mipango, Shogholo Msangi, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa NSSF, mjini Kigoma.
Baadhi ya wafanyabiasha wa Kigoma Mjini, wakimsikiliza kwa makini waziri wa fedha na Mipango, Mhe. Dkt Philip Mpango (Mb), wakati wa mkutano na Waziri huyo kuhusu masuala mbalimbali ya biashara na ulipaji kodi, mkutano uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa NSSF, mjini Kigoma.
Mbunge wa Kigoma Mjini, Mhe. Zitto Kabwe (kushoto), akisisitiza jambo wakati akizungumza na Waziri wa Fedha na Mipango,Dkt. Philip Mpango (Mb), baada ya kumalizika kwa mkutano kati yake na wafanyabiashara wa mjini Kigoma, uliofanyika katika ukumbi wa mikutano wa NSSF, mjini Kigoma.
Waziri wa Fedha na Mipango, Mhe. Dkt. Philip Mpango (Mb), (kushoto) akipeana mkono na Mbunge wa Kigoma Mjini Mhe. Zitto Kabwe, mara baada ya kumalizika kwa mkutano kati ya Waziri huyo na wafanyabiashara wa Mkoa wa Kigoma uliofanyika katika ukumbi wa NSSF, mjini Kigoma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...