Tuzo za makampuni 100 ya kiwango cha kati nchini kutolewa leo katika hafla itakayofanyika kwenye ukumbi wa Mlimani City. Hayo yamebainishwa katika mkutano uliowakutanisha wadau wote walioshiriki katika mchakato huo pamoja na waandaaji na wadhamini uliofanyika jana katika hoteli ya Hyatt Regency jijini Dar es salaam. Mchakato huu uliratibiwa na KPMG na Mwananchi Communications Ltd na kudhaminiwa na Benki M.
Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya maeneo maalum ya uwekezaji nchini (EPZA) Kanali Mstaafu. Joseph Simbakalia akizungumza na wadau wa tuzo za makampuni 100 ya kiwango cha kati nchini katika mkutano wa wadau uliofanyika jana katika hoteli ya Hyatt Regency.Hafla ya ugawaji tuzo hizo itafanyika leo kwenye ukumbi wa Mlimani City. Wengine kutoka kushoto ni Mkurugenzi wa Sumaria Group Bwn Ankush Shah, Mkurugenzi mtendaji wa Research Solution Africa Bwn Jasper Grosskurth, Mkurugenzi mkuu wa Institute of Directors Bwn Said Kambi na mwendeshaji wa shughuli hiyo Taji Liundi.
Mkurugenzi Mkuu mteule wa Benki M Bi. Jacqueline Woiso akizungumza katika mkutano huo, Benki M ndio wadhamini wakuu wa mchakato huo unaoratibiwa na KPMG na Mwananchi Communications Ltd.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...