Waziri nchi ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, uratibu, bunge, vijana na watu wenye ulemavu) Mhe Jenister Mhagama ametoa siku saba kwa
taasisi za serikali, wizara,makampuni na watu binafsi kuhakikisha wanalipa
madeni wanayodaiwa na Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF)
Vilevile Waziri Mhagama imeiagiza Bodi za
wadhamini za mifuko mingine ya hifadhi ya jamii kuhakikisha wanawasukuma wadeni
wao kulipa madeni yote wanayodaiwa ili kuiwezesha mifuko hiyo kujiendesha kwa
ufanisi zaidi.
Waziri Mhagama alitoa tamko hilo mwishoni mwa wiki jijini Dar es Salaam alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni huku akitumia fursa hiyo kumuagiza Katibu Mkuu wa Wizara yake, Bw Erick Shitindi kuhakikisha uongozi wa mifuko hiyo unampatia ripoti ya hatua zilizochukuliwa dhidi ya wahusika wote walioshindwa kulipa madeni yao.
“Ninafahamu
fika kuna mikataba ambayo ilisainiwa na pande zote mbili kabla ya kutolewa kwa
hiyo mikopo na makubaliano mengine hivyo naomba basi mikataba hiyo itumike
kufanikisha agizo hili,’’ alisema.
Pia
alimuagiza Mwenyekiti
wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF Prof Samwel Wangwe kuhakikisha kwamba anampatia ripoti
muafaka ya utekezaji wa agizo hilo.
"Kwa niaba ya serikali, ninataka kuona kwamba wadaiwa wote wa mifuko hii bila kujali nafasi zao kiuchumi au kisiasa wanalipa madeni wanayodaiwa…hii lazima ijumuishe makampuni, wawekezaji na taasisi za serikali,’’ alisema.
"Kwa niaba ya serikali, ninataka kuona kwamba wadaiwa wote wa mifuko hii bila kujali nafasi zao kiuchumi au kisiasa wanalipa madeni wanayodaiwa…hii lazima ijumuishe makampuni, wawekezaji na taasisi za serikali,’’ alisema.
Awali,
Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Profesa Godius
Kahyarara alisema licha ya mfuko wake kufanikisha utekelezeaji wa miradi
mbalimbali ikiwemo majengo bado wateja wake wengi hawajalipa madeni wanayodaiwa
na mfuko huo ikiwemo watu binafsi, taasisi za serikali na zile binafsi wakiwemo
pia wale walionunua nyumba za shirikal hilo.
Kwa
mujibu wa Prof. Kahyarara, shirika hilo bado linadai takribani sh bilioni 20
kutoka kwa wa wapangaji wake, deni linalohusisha pia dola za kimarekani milioni
1.2.Kiasi
kingine cha bilioni 86 kinadaiwa kama adhabu kutoka kwa waajiri walioshindwa
kuwasilisha michango ya wafanyakazi wao.
Madeni mengine ni pamoja na deni la sh milioni
42 na Dola za kimarekani milioni 35.9 ambazo zilitolewa kama mikopo kwa sekta binafsi mbalimbali huku
mkopo mwingine wa sh bilioni 38
ulitolewa kupitia SACCOS na bado hazijarejeshwa.
“Hata hivyo tumeanza kuchukua hatua mahususi kwa kulingana na matakwa ya sheria kuhakikisha kwamba madeni yote yanalipwa,’’ alibainisha Prof Kahyarara.
“Hata hivyo tumeanza kuchukua hatua mahususi kwa kulingana na matakwa ya sheria kuhakikisha kwamba madeni yote yanalipwa,’’ alibainisha Prof Kahyarara.
Kwa
mujibu wa Mkurugenzi Mkuu huo kufuatia mikopo hiyo shirika litachukua hatua
dhidi wadeni wake hatua iliyosababisha
baadhi ya wadaiwa hao kwenda mahakamani kupinga huku uamuzi wa mahakama kuhusu
suala hilo ulitarajiwa kutolewa leo (Jumatatu).
Akiwa
kwenye miradi ya shirika hilo Waziri Mhagama alionyesha kuridhishwa na miradi
hiyo iliyoanza mwaka 2014 na inatarajiwa kukamilika mwisho mwa mwaka 2016
ukihusisha ujenzo wa nyumba 439 ambazo zitauzwa kwa bei nafuu zikiwemo zile
ambazo zitapangishwa.
Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu Mhe. Jenister Mhagama akizungumza na uongozi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara (kulia) na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF Prof Samwel Wangwe.
Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu Mhe. Jenister Mhagama akiwa ameambatana na uongozi wa Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF) alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF Prof Samwel Wangwe. (kushoto) akizungumza mbele ya Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu Mhe. Jenister Mhagama wakati waziri huyo alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara (kulia).
Mkurugenzi mkuu wa NSSF, Profesa Godius Kahyarara (kulia) akizungumza mbele ya Waziri nchi ofisi ya waziri mkuu sera, uratibu, bunge ,vijana na watu wenye ulemavu Mhe. Jenister Mhagama wakati waziri huyo alipotembelea miradi ya nyumba za NSSF iliyopo wilayani Kigamboni mwishoni mwa wiki. Wengine ni pamoja na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa NSSF Prof Samwel Wangwe (kushoto).
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...