Shirika la Wanawake katika Sheria na Maendeleo Afrika (WILDAF) limewasilisha mapendekezo kwa Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria likitaka kufutwa kwa sheria mbalimbali za kimila zinazosimamia masuala ya mirathi ambazo zinalalamikiwa kuwakandamiza wanawake nchini . 

Akizungumza katika makabidhiano hayo Mkurugenzi wa WILDAF Bi. Judith Odunga amesema mapendekezo hayo yanataka kufutwa kwa sheria za kimila ambazo kwa kiasi kikubwa zimekuwa zikiwakanadamiza wanawake na kuwanyima haki ya kumiliki mali na kufanyiwa vitendo vya kidhalilishaji pale wanapofiwa na waume zao. 

Amesema katika mapendekezo hayo WILDAF inaiomba Serikali itunge sheria moja ambayo pamoja na zile za kidini itashughulikia masuala ya mirathi na kuweka usawa wa kisheria katika urithi wa mali kati ya mwanamke na mwanaume ikiwa ni pamoja na watoto wa kiume na wa kike kuwa na usawa katika kurithi mali inapotokea mzazi wa kiume amefariki. 

“Tulipoonana na Mhe Waziri Dkt Mwakyembe alituagiza kama tunataka kuwasaidia wanawake nchini basi tuwasilishe wizarani mapendekezo yetu juu ya nini kifanyike, sasa leo tumekuja hapa kutekeleza agizo la Mhe Waziri, tunampatia Katibu Mkuu mapendekezo husika, ambayo kwa asilimia kubwa yanapendekeza kufutwa kwa sheria zote za kimila ambazo zinamkandamiza mwanamke na mtoto wa kike na kutungwa kwa Sheria moja itakayoshughulikia masuala yote ya mirathi nchini na tuna imani kuwa yatafanyiwa kazi na kufanikisha azma ya WILDAF ya kuwasaidia wanawake nchini, alisema Mwenyekiti wa WILDAF Bi. Judith Odunga 

Akipokea mapendekezo hayo Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome ofisini kwake jijni Dar es Salaam amewapongeza na kuwashukuru WILDAF kwa kazi nzuri wanayoendelea kuifanya ili kuwasaidia wanawake na Serikali kwa ujumla wake kwani kitendo hicho kitasaidia sheria husika kufanyiwa marekebisho yatakayostahili ili ziendane na wakati, zikidhi mahitaji na kutafsiriwa katika lugha ambayo wananchi wengi ambao ndio walengwa wazielewe sheria hizo 

Amesema sasa Serikali imedhamiria kuhakikisha kuwa sheria zote nchini zinatafsiriwa na zile zinazotungwa zitakuwa kwa Kiswahili na Kingereza, uamuazi ambao utawawezesha watanzania wengi kuzielewa sheria hizo. 

Prof Mchome alaiwashukuru WILDAF kwa kazi waliyoifanya na kuwaadi kuwa wataalamu wake wizarani watayafanyia kazi mapendekezo yaoi ili kuhakikisha gurudumu la sheria nchini linasonga mbele na kuwasaidia wananchi wengi na kuwataka wadau wengine kuja wizarani kuzungumza pale watakapoona kuna haja ya kufanya hivyo kwani wizara ipo tayari kuwasilikiza na kuyafanyia kazi mapendekezo yao. 



Mkurugenzi wa WILDAF Bi. Judith Odunga akipeana mkono na Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome ofisini kwake jijni Dar es Salaam baada ya kupokea mapendekezo hayo yanayotaka kufutwa kwa sheria za kimila nchini ambazo zinadaiwa kuwakandamiza wanawake kwa kuwanyima haki sawa ya kumiliki mali pindi wanapofiwa na waume au wazazi wao anaeshuhudia kushoto ni Bibi Thabita Siwale Mwenyekiti wa Kikosi cha kupambana na haki za mirathi Tanzania- KIKUHAMI.

Wajumbe mbalimbali wa WILDAF walioambatana na Mwenyekiti kushuhudia uwasilishaji wa mapendekezo yao wakimsikiliza Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria Prof Sifuni Mchome Ofisini kwa jijini Dar es Salaam

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...