Watumishi wa Umma mkoani Dodoma wamefurika
katika vituo vya usajili kufuatia tamko la Serikali la kuongeza muda wa
usajili Vitambulisho vya Taifa kufikia Oktoba 31, 2016 ambapo mfanyakazi
au mwajiri ambaye atashindwa kutekeleza agizo hilo hatua stahiki
zitachukuliwa dhidi yake; tamko lililotolewa na Waziri ofisi ya Rais
Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora alipokutana na vyombo
vya habari hivi karibuni.
Watumishi waliojitokeza katika vituo wameonekana kuwa tayari wamejaza fomu za maombi ya Vitambulisho vya Taifa wakiwa wamejipanga kupigwa picha.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi amekuwa miongoni mwa viongozi waliotembelea moja wapo ya vituo vya usajili mkoani Dodoma; kushuhudia namna shughuli za usajili zinavyofanyika na kupata taarifa ya mpango wa utekelezaji zoezi hilo ilivyopangwa na mkoa husika, katika kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa wakati na kila mtumishi anasajiliwa na kuchukuliwa alama za Vidole, saini ya kielektroniki na picha.
Zoezi la Usajili Watumishi wa Umma linaenda sambamba na kuanza kwa uhakiki wa taarifa za uraia wa waombaji wote walioomba kupatiwa Vitambulisho vya Taifa.
Tayari mikoa ambayo usajili umekamilika, zoezi la uhakiki wa taarifa na mapingamizi linaanza mara moja ili vitambulisho kuanza kuzalishwa.
Watumishi waliojitokeza katika vituo wameonekana kuwa tayari wamejaza fomu za maombi ya Vitambulisho vya Taifa wakiwa wamejipanga kupigwa picha.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi amekuwa miongoni mwa viongozi waliotembelea moja wapo ya vituo vya usajili mkoani Dodoma; kushuhudia namna shughuli za usajili zinavyofanyika na kupata taarifa ya mpango wa utekelezaji zoezi hilo ilivyopangwa na mkoa husika, katika kuhakikisha zoezi hilo linakamilika kwa wakati na kila mtumishi anasajiliwa na kuchukuliwa alama za Vidole, saini ya kielektroniki na picha.
Zoezi la Usajili Watumishi wa Umma linaenda sambamba na kuanza kwa uhakiki wa taarifa za uraia wa waombaji wote walioomba kupatiwa Vitambulisho vya Taifa.
Tayari mikoa ambayo usajili umekamilika, zoezi la uhakiki wa taarifa na mapingamizi linaanza mara moja ili vitambulisho kuanza kuzalishwa.
Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, Meja Jenerali Projest Rwegasira akipokea ripoti ya utekelezaji wa zoezi la Usajili watumishi wa Umma toka kwa Afisa Usajili mkoa wa Dodoma Bwana Khalid Mrisho.
Afisa Utawala Bi. Salma Mohamed toka ofisi ya Wakala wa Geolojia (GST) akihakiki orodha ya watumishi wake ambao hawajasajiliwa Vitambulisho vya Taifa, kufuatia agizo la Serikali la kila mtumishi wa Umma kuwa amesajiliwa kufikia Oktoba 31, 2016. Pembeni ni Bi.Rehema Kionaumela Kaimu Mkuu wa Kitengo cha Uratibu Wilaya NIDA
Afisa Usajili NIDA Bw. Devis Lubago, akimsajili na kuchukua alama za kibaiolojia mtumishi wa Umma aliyefika ofisi za NIDA Dodoma kukamilisha usajili.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...