Na Emmanuel Massaka,Globu ya Jamii
SHIRIKISHO la soka nchini TFF limesema kuwa ligi kuu ya Wanawake inatarajia kuanza Novemba mosi mwaka huu katika viwanja mbalimbali nchini.
Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam leo Ofisa habari wa TFF,Alfred Lucas, amesema kuwa licha ya kukamilika kwa taratibu zote bado kuna tatizo la fedha kutokana kukosa kwa mdhamini wa ligi hiyo.
Lucas amesema kuwa timu zote zipo tayari licha yakuwepo kwa malalmiko kadha na rufaa za usajili kwa wachezaji kwa baadhi ya timu kuzilalamikia timu zingine kuchukua wachezaji wao.
Alizitaja timu ambazo zitashiriki katika ligi kuwa kutakuwa na makundi mawili ambapo kundi A zipo Viiva Queen ya Mtwara ,Mburahati Queen ya Dar es Salaam,Fair Play ya Tanga,Ever Green Dar es Salaam,Mlandizi Queen ya Pwani na JKT Queen ya Dar es Salaam.
Kundi B Marsh Academy ya Mwanza,Baobab Queen Dodom,Majengo Women Singida,Sisters Fc Kigoma,Kagera Queens na Panama Fc.
Ofisa habari wa TFF,Alfred Lucas, akizungumza na waandishi wa habari kuhusu Ligi ya wanawake itakayoanza kutimua vumbi Novemba Mosi kwaka huu ,jijini Dar es salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...