Na Humphrey Shao, Globu ya Jamii Ileje.

Wakazi wa Kata ya Bupigu Wilayani Ileje wameiomba Serikali kuongeza nguvu katika kilimo cha umwagiliaji kwa wakazi wa eneo hilo ili kupunguza tatizo la njaa wilayani humo.

Hayo yamesemwa na Katibu wa kikundi Nguvu kazi, Isaka Kamwela, kinachojihusisha na kilimo cha umwagiliaji katika kata hiyo kwenye Mto Mtumbisi.

“tumekuwa tukilima kwa kumwagilia kwa kipindi cha misimu minne kwa mwaka hali inayowafanya wakulima kuwa na fedha za kujikimu lakini uzalishaji umekuwa mdogo kutoka na kukosa elimu ya kutosha juu ya kilimo hicho” amesema Kamwela.

Amasema kuwa wamekuwa wakikutana na changamoto nyingi sana hasa za masoko pindi wanapolima bidhaa za mbogamboga na kuishia kuoza mashambani bila kupata wateja.

Amaeongeza kuwa ni vyema serikali ikawatuma wataalam wa masuala ya usindikaji mazao kwenda kutoa elimu ya kutosha kupunguza hasara wanayopata wa kulima .
 Mmoja wa wakulima wa kikundi cha Nguvu Kazi akipalilia Mahindi yae 
  Katibu wa kikundi Nguvu kazi, Isaka Kamwela alipokuwa akizungumza na Mwandishi wa Blobu hii namna wanavyoshiriki kwenye kilimo cha umwagiliaji
sehemu  ya wana kikundi cha umwagiliaji cha nguvu kazi wakiendelea na shughuli yao ya kilimo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...