Taarifa zilizoripotiwa na Kituo cha Televisheni ya Taifa ya nchi ya Cuba,  na kutangazwa moja kwa moja na Rais wa nchi hiyo, Raul Castro, zinaeleza kuwa Raiswa zamani wa nchi hiyo, Fidel Castro aliyekuwa na umri wa Miaka 90 na ambaye aliiongoza Cuba kwa zaidi ya miaka 30 kabla ya kuachia kijiti kwa mdogo wake Raul Castro (Rais wa sasa) mwaka 2008 amefariki Dunia ikiwa ni siku moja tu kuwaaga wajumbe wa Chama Cha Kikomunisti Cuba na kuwaambia atafariki siku si nyingi lakini mapinduzi yataishi, ikiwa ni baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Fidel Castro ambaye aliwahi kuiongoza nchi ya Cuba kama Waziri Mkuu kwa kipindi cha miaka 18 (kuanzia mwaka 1959 hadi mwaka 1976) kabla ya kushika nafasi ya Urais aliyodumu nayo kuanzia mwaka 1976 hadi mwaka 2008.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...