Asasi
Ya Vijana, Tanzania Youth Vision Association kwa Kushirikiana Na
International Republican Institute zimetoa mafunzo ya kuboresha Uwezo wa
Vijana kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba nchini katika Mikoa
mitatu ilijumuisha Wilaya Nne, ikiwemo Kinondoni, Dodoma Mjini, Chamwino
Na Tanga Mjini.
Mafunzo hayo yameweza kufikia vijana 500 kwa njia ya Warsha na Vijana aa wananchi zaidi ya 100,000 kupitia mitandao ya kijamii.
Lengo
kuu la Mafunzo hayo ni kuongeza uelewa na ushiriki wa Vijana katika
mchakato wa Mabadiliko ya Katiba. Katika ufunguzi wa mafunzo hayo,
Katibu Mtendaji wa TYVA ndugu Saddam Khalfan alisema, TYVA inaamini
Katiba ni Sheria mama na mwongozo ambao una uhusiano wa moja kwa moja na
maisha yetu ya kila siku.
Alibainisha
watu wengi wamekua wakisoma au kuisikia Katiba, na wengine wakidhani
Katiba ni maalumu kwa ajili ya wanasheria au wasomi tu. Kuna uhusiano
mkubwa kati ya Katiba bora ya Nchi, Demokrasia na Maendeleo ya Jamii.
Mwanaharakati
Na Mtetezi wa HAKI za Binadamu ndugu Deus Kibamba alipata kuwaelezea
washiriki wa mafunzo hayo historia ya mchakato wa mabadiliko ya Katiba,
Ushiriki wa wananchi katika mchakato wa Katiba, hatua muhimu katika
Mchakato wa utengenezaji Katiba, Mambo ya Msingi yaliyomo katika Katiba
inayopendekezwa na Mambo muhimu kuelekea kura ya Maoni ya Katiba
Inayopendekezwa.
Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania Bw, Deus Kibamba akitoa elimu kuhusu mchakato wa mabadiliko ya Katiba pamoja na historia ya mchakato huo kwa vijana wa wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.
Afisa wa IRI, Tony Alfred akizungumza jambo wakakati wa mafunzo ya mchakato wa mabadiliko ya Katiba kwa vijana wa wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma.
Makamu mwenyekiti wa TYVA, Kamala Dickson akizungumza jambo kwenye mkutano huo.
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...