Hatua ya TFF imekuja baada ya kuibuka malalamiko kutoka timu ya mpira wa miguu yaPanone ya Moshi Kilimanjaro kushangazwa na mchezaji huyo kuibukia timu ya Kagera ilihali akidaiwa kuwa na usajili katika timu hiyo kwa msimu wa pili mfululizo.

Kwa haraka, Idara ya Mashindano ya TFF imebaini kuwa mchezaji huyo alikuwa na usajili kwa timu zote mbili kwa usajili wa majina tofauti ilihali picha ikionekana kuwa mmoja.

Panone FC alisajiliwa kwa jina la Christopher Mshanga kuanzia msimu wa 2015/2016 na pia msimu wa 2016/17.
Taarifa za awali ambazo TFF ingali ikizifanyia kazi zinasema kwamba baada ya kusajili Panone FC ya Moshi, akachezea timu mbili na kuaga kuwa amekwenda kutibiwa majeraha, lakini wakati anasubiriwa, amekuja kuonena kwenye mchezo ambao Kagera ilikuwa ikicheza na Young Africans kwenye ligi ya vijana wa U20 ya TFF.

Kwa mbinu za kuchezea mtandao, mchezaji huyo pia akasajiliwa na Kagera Sugar msimu wa 2016/17 na Kagera kwa jina la Christopher Paschal Peter Mshanga.




leseni ya mchezaji huyo akionekana akiwa amesajiliwa Panone FC inayoshiriki ligi daraja la kwanza.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...