Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Thamini Uhai Dk.Nguke Mwakatundu (kulia) akikabidhi moja ya pikipiki tisa zenye thamani ya shilingi milioni 40 Kwa Mganga Mkuu wa mkoa Kigoma Dk.Paul Chaote kwa niaba ya Katibu tawala wa mkoa Kigoma Charles Palangyo ambao pikipiki hizo zitatumika kwenye vituo vya afya mkoani humo.
Mganga Mkuu wa mkoa Kigoma Paul Chaote (kushoto) akikabidhi funguo ya pikipiki kwa Vitus Bukombe Mganga Mfawidhi wa kituo cha afya Ilagala (kati kati) ikiwa ni moja ya pikipiki tisa zilizotolewa na shirika la Thamini Uhai kwa vituo vya afya mkoani Kigoma kwa ajili ya kusaidia kampeni ya kukabiliana na vifo vya mama wajawazito na watoto wakati wa kujifungua anayeshuhudia kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Thamini Uhai Dk.Nguke Mwakatundu.
Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Thaimini Uhai Dk.Nguke Mwakatundu (wa pili kulia mstari wa mbele) akiwa katika picha ya pamoja na wageni waliohudhuria hafla ya makabidhiano ya pikipi tisa zenye thamani ya shilingi milioni 40 zilizotlewa na shirika hilo kwa serikali ya mkoa Kigoma (wa pili kushoto mstari wa mbele) Mganga Mkuu wa mkoa Kigoma,Dk.Paul Chaote. (Picha Zote na Fadhili Abdallah).
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...