Msafara wa Waziri wa Ardhi, ukiwa umewasili katika jengo la Halmashauri ya wilaya ya Kishapu Mkoani Shinyanga kwa ajili ya kukutana na wakuu wa idara hususani wa sekta ya ardhi wa Kishapu kabla ya kwenda katika mkutano wa kusikiliza kero za wananchi katika mji wa Mhunze.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimkabidhi vitabu vyenye muongozo namna ya kupanga miji sambamba na kitabu chenye majina 33 ya makampuni yaliyojitolea kushirikiana na serikali kupima ardhi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akitatua mgogoro wa ardhi wa wananchi wa Kishapu waliokuwa wanagombea eneo la makazi.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akitatua mgogoro wa ardhi wa Bibi Safina Ibrahim mara baada ya kuleta vielelezo vyake.
Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi Mhe. William Lukuvi akimhoji Mthamini wa wilaya ya Kishapu Reuben Lauwo (mwenye shati ya bluu) na Afisa Ardhi wa wilaya ya Kishapu Grace Pius (gauni la kitenge) kwanini hawakumlipa fidia bwana Daudi Amos (wa kwanza kushoto) kama inavyostahiki. Kwa taarifa kamili na picha zaidi BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...