Mtanzania Felistas Joseph, amechaguliwa kuongoza Kamati ya nchi za Maziwa Makuu ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari (International Conference on Great Lakes Region –ICGLR).
Bibi Felistas amechaguliwa kuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo katika uchaguzi uliofanyika mjini Pointre Noire, nchini Congo Desemba Mosi mwaka 2016. Kamati iliyoundwa chini ya Itifaki ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari inajumuisha wajumbe 12 kutoka nchi wanachama wa ICGLR  ambapo wajumbe hao huidhinishwa na Baraza la Mawaziri la ICGLR (Regional Inter-Ministerial Council- RIMC).
Bibi Felistas ni Mkurugenzi  Msaidizi  katika Idara ya Huduma za Kisheria kwa Umma Wizara ya Mambo ya Katiba na Sheria na amekuwa Mwenyekiti wa Kamati ya Kitaifa ya Tanzania ya Kuzuia Mauaji ya Kimbari tangu ilipoundwa mwezi Februari mwaka 2012.
Katika nafasi yake ya Mwenyekiti wa Kamati ya Kanda, Bibi Felistas atasaidiwa na Makamu Mwenyekiti kutoka nchini Burundi, Katibu kutoka DRC ambao kwa pamoja wanatarajiwa kuthibitishwa na Baraza la Mawaziri la ICGLR  katika kikao chao kitakachofanyika wiki mbili  zijazo nchini Kenya.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...