Rais na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi
ya Ulinzi na Usalama Tanzania Mh. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli amewapandisha
vyeo Maafisa Wakuu wawili wa JWTZ kuwa Meja
Jenerali kuanzia tarehe 03 Disemba
2016. Maafisa Wakuu hao ni;
Brigedia Jenerali George William Ingram
ambaye ni Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga, na Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo
ambaye ni Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa.
Mkuu wa Kamandi ya Jeshi la Anga
Brigedia Jenerali Michael Wambura Isamuhyo
Mkuu wa Jeshi la Kujenga Taifa
Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi Jenerali
Davis Adolf Mwamunyange kwa niaba ya Rais na Amiri Jeshi Mkuu anawapongeza na
kuwatakia kheri katika vyeo vyao vipya.
Imetolewa na
Kurugenzi ya Habari na
Uhusiano Makao Makuu ya Jeshi, Upanga
S.L.P 9203, Dar
es Salaam, Tanzania.
Kwa Mawasiliano zaidi: 0784-477638/0756-716085
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...