Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu)
Mhe. Jenista Mhagama ameshauri uongozi wa Chama cha Akiba na Mikopo cha
Ofisi ya Waziri Mkuu (Makamu Saccos) kuwa na ubunifu katika
utendaji ili kuleta manufaa zaidi kwa wanachama wake.
Mhe.
Mhagama ameyasema hayo wakati wa Mkutano Mkuu wa Mwaka wa Wanachama wa
Chama hicho uliofanyika Januari 19, 2017 mkoani Dodoma.
Katika
Mkutano huo Mhe. Waziri alisisitiza kuwepo na mikakati madhubuti ya
kubuni miradi itakayowezesha chama kuwa na vyanzo vyake vya mapato na
kuwa na mikakati ya kuongeza wanachama wapya kwa kuzingatia umuhimu wa
chama hicho.“Ni
muhimu kuwa na mikakati madhubuti ya kubuni miradi, kuongeza wanachama
pamoja na kuwa na vitu vya kiupekee na vya kiufanisi vitakavyokisaidia
chama kuwa imara katika utendaji wake”, alisema Waziri Mhagama.
Aliongeza
kuwa chama hicho kimekuwa msaada mkubwa kwa wanachama wake amabapo
wengi wao wamekuwa na maendeleo mbalimbali kutokana na uwepo wa fursa za
mikopo isiyokuwa na masharti magumu.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu)
Mhe. Jenista Mhagama (katikati) akisalimia wanachama waChama
cha Akiba na Mikopo Ofisi ya Waziri Mkuu (hawapo pichani) wakati wa
Mkutano wao wa mwaka Uliofanyika Ukumbi wa Mikutano Ofisi ya Waziri Mkuu
Dodoma tarehe 19 Januari, 2017.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na Watu wenye Ulemavu)
Mhe. Jenista Mhagama akizungumza jambo wakati wa Mkutano Mkuu wa mwaka
wa Wanachama wa Chama cha Akiba na Mikopo Ofisi ya Waziri Mkuu Januari
19,2017 katika Ukumbi wa Ofisi ya Waziri Mkuu Dodoma.
Baadhi
ya wajumbe Chama cha Akiba na Mikopo Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia
maelekezo ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Ajira na
Watu wenye Ulemavu) Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) wakati wa
Mkutano wa kwanza wa mwaka Januari 19, 2017 Mkoani Dodoma.
Mkurugenzi
Idara ya Utawala na Usimamizi wa Rasilimali Watu Ofisi ya Waziri Mkuu
Bw.Issa Nchasi akizungumza jambo wakati wa Mkutano wa Mwaka wa Wanachama
wa Akiba na Mikopo wa Ofisi hiyo Mkoani Dodoma Januari 19, 2017.
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
PICHA ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...