Na Humphrey Shao,Globu ya Jamii .

Naibu Meya wa Manispaa ya Ilala na Diwani wa Vinguti , Omary Kumbilamoto, ameahidi kuendelea kushirikiana na wakazi wa kata hiyo hili kuakikisha wanapata maendeleo. 

Kumbilamoto amesema hayo alipokuwa akizungumza na wakazi wa mtaa wa Kaza buti kata ya Vingunguti wakati akikabidhi vifaa vya michezo na mabati kwa tasisi ya Makazi kazi na vikundi vya michezo. 

“nitoe shukrani kwa wakazi wa eneo la kazabuti kwa jinsi mlivyoweza kuniamini katika uchaguzi mkuu mwaka jana na kunipa fursa ya kuwa Diwani wenu na leo nimekuja kuwatembelea kwa ajili ya kutimiza moja ya ahadi zangu hivyo naomba niwaambie kuwa nitakuwa nanyi bega kwa bega katika kuakikisha kuwa tunaleta maendeleo katika kata yetu” amesema Kumbilamoto. 

Kumbilamoto amesema kuwa amemaliza mwaka mmoja ndani ya utawala wake kwa kuweza kutimiza ahadi kadhaa ambazo aliahidi ikiwemo ununuzi gari ya kubebea wagonjwa , Mashine yakufulia katika Zahanati ya vingunguti na ujenzi wa choo kwa ajili ya wodi ya kinamama wajawazito. Aidha ametaja kuwa pia katika mwaka huu mmoja maeweza kuwasaidia wanawake wajasilimali ambao aliwapa vyerehani viwili hiki kuendeleza vikundi vyao. 

Kumbilamoto alimaliza kwa kuwataka wakazi wa Vingunguti kuwa wachapakazi kwa kila jambo kama Rais wanchi Dkt John Pombe Magufuli. 
Mwenyekiti wa Haki za Binadamu wa Chama cha Wananchi (CUF) Mohamed Mluya, akikabidhi jezi kwa vikundi vya Joging.
Naibu Meya wa Manispa aya Ilala, Omary Kumbilamoto, akikabidhi jezi kwa kikundi cha Makazi Kazi kilichopo katika mtaa wa Kaza Buti
Naibu Meya na wenzie wakicheza muziki mara baada ya kumalizika kwa mkutano huo
Wananchi wakifatilia mkutano huo kwa makini

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...