Waziri wa Ujenzi,
Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa ameitaka Menejimenti ya Mfuko wa
Mawasiliano kwa wote (UCSAF), kuhakikisha vijiji vyote nchini ambavyo havijaunganishwa
na huduma ya mawasiliano vinaunganishwa
kabla ya mwisho wa mwaka huu.
Aidha, Profesa Mbarawa
amesisitiza mfuko huo kutoa kipaumbele kwa vijiji vyote vilivyomo sehemu za
mipakani ili kuimarisha ulinzi na uharaka wa mawasiliano katika maeneo hayo.Amewaagiza
UCSAF
kukutana na mitandao ya simu ili kukamilisha kazi kwa mujibu wa mkataba
kwa kata 121 ambazo hazijapata huduma ya mawasiliano hapa
nchini.
“Nia ya Serikali ni kuhakikisha vijiji vyote
nchini vinapata huduma ya mawasiliano ifikapo mwishoni mwa mwezi Novemba ili
kuwezesha mikakati mingine ya kuboresha Mifumo ya Tehama katika shule na
Hospitali kuendelea na hivyo kuhuisha huduma za Tehama katika Sekta za afya na
elimu”, amesema Profesa Mbarawa.
Profesa Mbarawa
ameonya kampuni za simu zitakazoshindwa kupeleka mawasiliano katika maeneo
waliyopangiwa kwa wakati zitapokonywa masafa katika maeneo husika ili kuzipa
kampuni zilizo tayari.
Naye Mjumbe wa Bodi ya
UCSAF Bw. Godfrey Simbeye, amemhakikishia Waziri Mbarawa kuwa Bodi yake
imejipanga kuhakikisha inaratibu huduma zote za Tehama zinazotolewa na taasisi
mbalimbali nchini ili kuweka uwiano wa huduma hizo nchini kote.
Kwa upande wake, Mtendaji
Mkuu wa UCSAF Eng Peter Ulanga, amesema kuwa mfuko huo umejipanga kupeleka
mawasiliano katika maeneo yasiyo na mvuto kibiashara ili kutoa haki kwa wakazi
wa maeneo hayo kunufaika na fursa za mawasiliano na kuchochea maendeleo.
Takribani asilimia 94
ya Wakazi wa Tanzania wanapata huduma ya mawasiliano lengo likiwa ni kufikia
asilimia 100 ifikapo mwishoni mwa mwaka huu.
Imetolewa
na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa, akikagua kumbukumbu za wateja wanaohudumiwa na kampuni ya simu TTCL kanda ya Kaskazini eneo la Kijitonyama jijini Dar es salaam.
Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa (Katikati), akisisitiza jambo kwa maofisa wa kampuni ya Simu TTCL kanda ya Kaskazini alipokagua huduma zinazotolewa na kampuni hiyo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...