Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli ambaye bia yake ndio mdhamini mkuu wa Kilimanjaro Marathon amewataka washiriki wa mbio hizokujisajili mapema ili kuepuka na msongamano dakika za mwisho.

Alitoa rai hiyo Jijini Dar es Salaam huku akisema mbio hizo zimekuwa kubwa na maarufu na hivi kuwavutia washiriki wengi  jambo ambalo linalazimu washiriki waanze kujisajili mapema.

“Mwaka jana kulikuwa na wakimbiaji zaidi ya 8000 kutoka nchi zaidi ya 45 na tunatarajia kupata washiriki wengi zaidi mwaka huu,” alisema na kuongeza kuwa Kilimanjaro Premium Lager inajivunia kuwa mdhamini mkuukwa miaka 15 mfulululizo sasa.
Meneja wa Bia ya Kilimanjaro Premium Lager, Pamela Kikuli akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kuhusu Kilimanjaro Marathon 2017. Wengine mini mbio za kilometa 5, Meneja Masosko wa Grand Malt Tanzania kutoka kushoto ni Meneja wa Grand Malt, Oscar Shelukindo anayedhamini mbio za kilometa 5, Meneja Masoko wa GAPCO Tanzania Caroline Kakwezi-kilometa 10 kwa watu wenye ulemavu na Mkurugenzi wa Tigo Kanda ya Kaskazini, George Lugata-kilometa 21.

Alisema wakati wa msimu huu wa Kilimanjaro Marathon, Kilimanjaro Premium Lager itaanza kuuzwa katika chupa mpya yenye ujazo wa mililita 375 kwa Kilimanjaro na Arusha.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...