Na Lorietha Laurence-WHUSM
Serikali imeunga mkono uwanzishwaji wa Bodi ya Maendeleo ya Mpira wa Miguu (TDF) wenye lengo la kuratibu vyanzo mbalimbali vya mapato ili kutekeleza maendeleo ya mpira nchini ikiwemo kukuza vipaji vya michezo kwa vijana wa kike na wa kiume.
Hayo yamesemwa na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye alipozindua Bodi hiyo iliyo chini ya uratibu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania leo Jijini Dar es Salaam ambapo aliwataka wadau wa michezo,wananchi na sekta binafsi kuunga mkono jitihada hizo.
“Jambo hili ni jema sana katika sekta ya michezo nchini hivyo ni jukumu letu sote kuhakikisha tunaunga mkono juhudi hizi zenye lengo la kuleta matokeo chanya katika sekta hii muhimu mfano mzuri ni vijana wetu wa Serengeti Boys wameshatuonyesha kuwa tunaweza kufika mbali” alisema Waziri Nnauye.
Aidha, aliitaka Bodi hiyo kufanya kazi kwa uadilifu na uaminifu ili kuhakikisha mfuko huu unakua na hivyo kuwezesha utendaji fanisi wa kukuza vipaji vya michezo wa kike na wa kiume na kwa wale watakaokiuka miiko ya kazi uongozi usisite kuchukua hatua za kinidhamu dhidi yao.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye akiongea na wadau wa michezo katika ufunguzi wa Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) ulioanzishwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo Jijini Dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akimkabidhi nyaraka za Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) kwa Meneja wa PPF Kanda ya Ziwa Meshack Bandawe (kushoto), ambaye ni mjumbe wa bodi hiyo ,katikati ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.Jamal Malinzi.Leo Jijini dar es Salaam.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (kulia) akimkabidhi nyaraka za Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) kwa Meneja Mwandamizi wa Benki ya NBC Salmi Rupia(kushoto), katikati ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) Bw.Jamal Malinzi.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Nape Moses Nnauye (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wajumbe wa Bodi ya Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) mara baada ya kuuzindua leo Jijini Dar es Salaam .(Picha na Lorietha Laurence-WHUSM).
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
HABARI ZAIDI BOFYA HAPA
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...