Mbunge wa Geita Mjini Constatine Kanyasu amesikitishwa kwa kitendo cha wananchi waliokuwa wamejenga kwenye hifadhi ya misitu kubomolewa huku wengine wakiachwa katika maeneo hayo na kuahidi kushughulikia ili haki itendeke sawa na wale ambao hawajabomolewa.

Hayo aliyasema kwenye mkutano wa hadhara ambao umefanyika kwenye mtaa wa Mwatulole kata ya buhala hala wilaya na Mkoa wa Geita,wenye lengo la kusikiliza na kutatua kero za wananchi katika jimbo ambalo analiongoza.

Mh Kanyasu amesema kuwa amesikitishwa na hatua ya TFS kubomoa nyumba za watu wengine huku wale wenye uwezo wakiachwa na kuendelea kukaa kwenye maeneo hayo kutokana na hilo wameagiza watu wa TFS kuangalia kama wale waliobomolewa pale yalikuwa ni maeneo yao na ninani ambaye aliwauzia.

“Naomba Nikiri na mimi iliniuma sana lakini kwa sababu ni serikali na sikuwepo na sijui kama walitumia sheria mimi naomba yeyote ambaye ni haki yake ya msingi alete na mimi nitashughulikia”Alisema Kanyasu

Hata hivyo Bi,Chausiku Lusetula ambaye ni miongoni mwa wanananchi waliobomolewa makazi yao amemuomba Mbunge kuwasaidia ili wapate haki zao za msingi na kwamba kwa sasa hawana makazi ya kuishi baada ya makazi yao kubomolewa.

“Mheshimiwa Mbunge sisi ni watu ambao tumekosa makazi kwa sasa hatujui ni wapi tutaishi na chakusikitisha kwanini sisi tubomolewe na wengine waendelee kukaa kwenye maeneo ambayo inasemekana ni hifadhi ya misitu kama ni hivyo ni vyema haki itendeke kwa wote”Alisema Chausiku

Diwani wa kata ya Buhala hala ,Mussa Kabese amewaambia wananchi kuwa mbunge wa jimbo la Geita Mjini tayari amekwisha mwandikia Waziri mwenye dhamana barua ambayo imemwomba matumizi ya pori la buhala hala kubadilishwa na kuwekwa taasisi ambazo zitawasaidia wananchi ambao wapo kwenye mitaa ya shinde na magogo kupata mahitaji ya msingi ikiwemo swala la elimu na afya.

Hatua hii imekuja ni baada ya takribani wiki mbili kumalizika ambapo wananchi ambao wamejenga kwenye hifadhi ya misitu inayosimamiwa na wakala wa misitu nchini TFS kubomolewa makazi yao.
Mbunge wa Jimbo la Geita Mjini ,Constatine Kanyasu,akizungumza na wananchi wa kata ya Buhala hala wakati aliipokwenda kusikiliza kero ambazo zimekuwa zikiwakabili kwenye maeneo ambayo wanaishi.
Maeneo ambayo wananchi walibomolewa nyumba zao.
Moja kati ya wananchi ambao wameuzulia Mkutano huo akielezea kero yake kwa Mbunge wa Geita mjini wakati wa Mkutano huo.
Meza kuu ikiongozwa na Mbunge wa Geita,Mjini,Diwani wa kata ya Buhala hala pamoja na baadhi ya wajumbe wakifatilia maelezo kutoka kwa wananchi.
Wananchi ambao walikuwa wamejitokeza kwenye mkutano huo wakisikiliza wakati Diwani wa kata ya Buhala hala alipokuwa akitoa maelezo na kujibu baadhi ya changamoto za wananchi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...