Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa akitoa hotuba yake ya ufunguzi katika mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma uliofanyika Ikulu, Dar es Salaam mapema leo. Mkutano huo uliandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Ofisi ya Msajili wa Hazina.
 Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango akizungumza katika mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ambao ulikuwa na lengo ya kujadili nafasi za Mashirika ya Umma katika utekelezaji wa Mpango wa II wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano.
 Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja akitoa ukaribisho kwa Watendaji Wakuu na Wenyeviti wa Bodi za Mashirika ya Umma kwa niaba ya waandaji wa mkutano huo uliofanikiwa kuleta pamoja wakuu wa mashirika zaidi ya 70 nchini.
Sehemu ya Wenyeviti na Wakurugenzi Watendaji wa Mashirika ya Umma wakifuatilia mkutano wa Wakuu wa Mashirika ya Umma ulioandaliwa na Taasisi ya Uongozi kwa kushirikiana na Tume ya Mipango na kufanyika Ikulu, Dar es Salaam mapema leo.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (aliyeketi katikati), Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (wapili kutoka kulia), Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja (wapili kushoto), Kaimu Msajili wa Hazina Bw. Mihalale Mwakibinga (kushoto) na Kaimu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Mipango Maduka Kessy (kulia) katika picha ya pamoja na Wenyeviti wa Bodi wa Mashirika ya Umma.
 Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa (aliyeketi katikati), Waziri wa Fedha na Mipango Mhe. Dkt. Philip Mpango (wapili kutoka kulia), Afisa Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Uongozi Profesa Joseph Semboja (wapili kushoto), Kaimu Msajili wa Hazina Bw. Mihalale Mwakibinga (kushoto) na Naibu Mtendaji Mkuu wa Tume ya Mipango Maduka Kessy (kulia) katika picha ya pamoja na Wakurugenzi Watendaji wa Mashirika ya Umma.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...