Na  Bashir  Yakub .
Ni  kweli ardhi  umenunua  kwa  hela  yako, ni kweli kiwanja  umetafuta  mwenyewe, ni kweli wewe  ni  Mtanzania  wala sio  mgeni,  lakini  pia  ni  kweli  ukubali  kuwa  ardhi  hiyo  unaimiliki  katika  kipindi  maalum  na  sio  moja  kwa  moja/milele.
 Hapo  ulipo  unapoita  nyumbani  kwako  unapamiliki  kwa  muda  maalum na  sio  moja  kwa  moja  kama  unavyodhani. Tanzania  hakuna  anayemiliki  ardhi  moja  kwa  moja  bali  wote  tunamiliki  kwa  muda  maalum.
Hati  ya  kumiliki  ardhi uliyonayo  au  unayotafuta  kupata   hutolewa  kwa  muda  maalum. Hakuna  hati  ya  milele  isipokuwa  kila  hati  inacho  kipindi  chake.   
Kipindi  kinapoisha  maana  yake  na  umiliki  wako umeisha.

 Tutaona  ufanye  nini  kipindi  kinapoisha na athari  za kuacha  kufanya  ulichotakiwa  kufanya baada  ya  kipindi  kuisha. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...