Na Bashir
Yakub
Kutelekezwa ni pamoja
na kunyimwa huduma
za muhimu ambazo
kama mke alistahili
kupata. Huduma muhimu ni
kama chakula, mavazi ,
makazi, matibabu, hela ya kujikimu kwa
matumizi ya kawaida
ya mwanamke, pamoja
na kila hitaji
ambalo kama mwanamke
alitakiwa kulipata.
Ifahamike kuwa habari
ya kutelekeza inawahusu wote
mke na mme
kwa maana ya kuwa
mme anaweza kumtelekeza
mke halikadhalika mke
anaweza kumtelekeza mme. Hata
hivyo makala yatazungumzia mme
kumtelekeza mke ambapo sura
ya 29 , Sheria ya
ndoa iliyofanyiwa marekebisho
mwaka 2010 itarejewa.
1.AINA ZA KUTELEKEZA.
( a ) Aina
ya kwanza ni kutelekeza
ambako mume anaondoka
kabisa ndani ya
nyumba ambayo alikuwa
akiishi na mke
wake kama wanandoa na
kwenda kuishi kwingine. Haijalishi huko alikoenda
panajulikana ni wapi au
hapajulikani suala la
msingi ni kwamba
hayupo katika makazi
yake ya kawaida
ya familia.
Aidha ikiwa hayupo
nyumbani lakini kwa
sababu za msingi
na za kisheria huko
sio kutelekeza. Sababu
hizo ni kama kuwa
jela, kuwa hospitali, kuwa amehamishiwa
sehemu nyingine kwasababu ya
matibabu kwa
mfano wengine huamishiwa
mikoani, na pia kuwa vitani
labda baadae mkapoteza
mawasiliano na mazingira
mengine ya dharula
za kibinadamu na
ambayo siyo ya
makusudi hayawezi kuitwa
kutelekeza.
( b ) Aina
nyngine ya kutelekeza ni
hatua ya kuwa
mme na mke
wanaishi wote katika
nyumba moja au
chini ya paa moja lakini
mume huyo hajishughulishi na
kutoa matumizi au
matunzo kwa mke
huyo kwa namna
yoyote ile. Hajui anakula
nini, hajui anavaa
nini, hajui anapata vipi
matibabu, kwa ufupi hajui
lolote zaidi ya
kumuona tu kama
binadamu wengine ambao
anawaona mitaani na
hana uhusiano nao.
Pia kuishi chini ya
paa moja lakini
vyumba tofauti nako
ni kutelekeza hata kama
mke anapewa matumizi
yote yanayostahili. Zaidi, hata
kulala chumba kimoja
lakini vitanda tofauti
kwa muda mrefu
tena kwa makusudi
kwasababu ya mgogoro
wowote nako ni kutelekeza. Lakini
pia kulala kitanda
kimoja bila kushiriki
tendo la ndoa kwa
makusudi kwa muda mrefu bila
sababu za msingi
za kiafya au vinginevyo nako ni
kutelekeza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...