Na Shamimu Nyaki-WHUSM.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe
ameliagiza Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) kusimamia mashindano ya Miss
Tanzania kwa ufanisi na kuhakikisha yanazingatia kanuni za uandaaji wa
mashindano ya urembo.
Mhe. Mwakyembe ameyasema hayo jana Mjini Dododma wakati alipokutana na
Kamati ya Miss Tanzania iliyoongozwa na mwenyekiti Bw Hashim Lundenga na
kuwataka kusimamia vyema shindano hilo ili kupata washindi wenye viwango
vinavyotakiwa Kimataifa.
“Nawaagiza BASATA simamieni shindano hili ili tupate washindi wenye viwango
watakaosaidia Tanzania kujitangaza Kimataifa katika urembo”, Alisema Mhe.
Mwakyembe.
Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Braza la Sana la Taifa (BASATA) Bw. Godfrey
Muingereza amemuahidi Mhe Waziri Mwakyembe kuwa atasisamia kwa karibu na
kwa ufanisi mashindano ya Miss Tanzania ili yawe na ubora zaidi utakaowezesha
nchi kufanya vizuri kwenye mashindano ya Dunia.
Naye Mweyekiti wa Kamati ya Miss Tanzania Bw. Hashim Lundenga ameahidi
kushirikiana na Wizara pamoja na BASATA katika kuandaa na kuboresha shindano
la Miss Tanzania ili kuwa na nguvu ya pamoja katika kupata ushindi utakaoletea
Taifa heshima.
Mashindano ya Miss Tanzania yanayotarajiwa kufanyika baadae mwaka huu
yanaandaliwa na kusimamiwa na Kamati inayoongozwa na Mwenyekiti Bw. Hashim
Lundenga, Katibu Wake Bw.Bosco Majaliwa na Mjumbe Bw. Deo Kapten.
Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Harrison
Mwakyembe(katikati) akiwa katika picha ya pamoja na Kamati ya Miss Tanzania mara
baada ya kufanya mazungumzo ofisini kwake Mjini Dododma jana.Wa kwanza kulia ni
Katibu Mtendaji wa Baraza la Sanaa la Taifa Bw.Godfrey Muingereza.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...